Ratiba ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi ya 2009
MAAGIZO
Katika mwaka wa 2009, Shule ya Huduma ya Kitheokrasi itaongozwa kwa kutegemea utaratibu ufuatao.
VICHAPO VITAKAVYOTUMIWA: Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya [bi12], “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa” (Toleo la 1992) [si], Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu [lr], na Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko (Toleo la 2004) [rs].
Shule inapaswa kuanza KWA WAKATI kwa utangulizi wa kuwakaribisha wasikilizaji kisha fuateni utaratibu ufuatao. Baada ya kila hotuba, mwangalizi wa shule atamkaribisha msemaji anayefuata.
MAMBO MAKUU YA USOMAJI WA BIBLIA: Dakika 10. Mzee, au mtumishi wa huduma anayestahili, atumie dakika nne za kwanza kuzungumzia mambo makuu ya usomaji wa Biblia wa juma hilo. Utaratibu huo utabadilika tu wakati usomaji wa Biblia wa juma hilo unaanza na sura ya kwanza ya kitabu cha Biblia. Wakati huo, anapaswa kutumia dakika nne za kwanza kuzungumzia mambo makuu kutoka katika kitabu “Kila Andiko.” Kwa mfano, sura tano za kwanza za Mwanzo zitazungumziwa juma linaloanza Januari 5, kwa hiyo msemaji anapaswa kuchagua mambo makuu machache kutoka katika mafungu ya kwanza ya sura inayozungumzia Mwanzo katika kitabu “Kila Andiko.” Anapaswa kutoa habari hiyo kwa njia itakayonufaisha kutaniko. Iwe anazungumzia usomaji wa Biblia wa juma hilo au mambo makuu kutoka kitabu “Kila Andiko,” lengo kuu ni kuwasaidia wasikilizaji waelewe ni kwa nini habari hiyo ni yenye manufaa na jinsi inavyowanufaisha. Msemaji anapaswa kuwa mwangalifu asipite zile dakika zake nne za kwanza. Anapaswa kuhakikisha kwamba anawaachia wasikilizaji dakika sita ili watoe maelezo mafupi yasiyozidi sekunde 30 kuhusu mambo yaliyowapendeza katika usomaji wa Biblia. Kisha mwangalizi wa shule atawaruhusu wanafunzi watakaotoa hotuba katika shule ya pili au ya tatu waondoke.
HOTUBA NA. 1: Isizidi dakika 4. Hii ni hotuba ya usomaji inayopaswa kutolewa na ndugu. Mwanafunzi anapaswa kusoma habari hiyo bila kutoa utangulizi wala umalizio. Mwangalizi wa shule atajitahidi hasa kuwasaidia wanafunzi wasome kwa njia inayoeleweka, wawe na ufasaha, wakazie maana kwa njia inayofaa, wawe na ubadilifu wa sauti, watue kwa njia inayofaa, na wasome kwa njia ya maongezi ya kawaida.
HOTUBA NA. 2: Dakika 5. Hotuba hii inapaswa kutolewa na akina dada. Akina dada wanaopewa mgawo huu watapewa au watajichagulia kikao katika orodha ya vikao iliyo kwenye ukurasa wa 82 wa kitabu Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi. Mwanafunzi anapaswa kutumia kichwa kilichoonyeshwa na kuonyesha jinsi habari hiyo inavyoweza kutumiwa katika utumishi wa shambani katika eneo lenu. Ikiwa chanzo cha habari hakijaonyeshwa, itambidi mwanafunzi afanye utafiti kuhusu habari hiyo katika vichapo vyetu. Mwangalizi wa shule ataangalia hasa jinsi mwanafunzi anavyoeleza habari hiyo na jinsi anavyomsaidia mwenye nyumba kuelewa maana ya Maandiko na mambo makuu. Mwangalizi wa shule atampa msaidizi mmoja.
HOTUBA NA. 3: Dakika 5. Hotuba hii inaweza kupewa ndugu au dada. Mwanafunzi anapaswa kuzungumzia kichwa kilichoonyeshwa. Ikiwa chanzo cha habari hakijaonyeshwa, itambidi mwanafunzi afanye utafiti kuhusu habari hiyo katika vichapo vyetu. Ndugu anapopewa hotuba hii, ataitoa kama hotuba kwa wasikilizaji kwenye Jumba la Ufalme. Dada anapopewa hotuba hii, ataitoa jinsi Hotuba Na. 2 inavyotolewa. Hakikisha kwamba akina ndugu tu ndio wanaopewa hotuba zenye vichwa vilivyo na alama ya nyota, na wakati wowote inapowezekana, hotuba hizo zipewe mzee au mtumishi wa huduma.
SHAURI: Dakika 1-2. Mwangalizi wa shule hatatangaza mapema sifa ya usemi ambayo mwanafunzi anafanyia kazi. Baada ya Hotuba Na. 1, Na. 2, na Na. 3, mwangalizi wa shule atatoa maelezo yanayojenga kuhusu jambo linalostahili kusifiwa katika hotuba hiyo, na kuonyesha sababu hususa zilizofanya jambo hilo liwe zuri akirejelea mara kwa mara kitabu Shule ya Huduma. Kulingana na uhitaji wa kila mwanafunzi, mashauri mengine yanaweza kutolewa faraghani baada ya mkutano au katika pindi tofauti ili kumsaidia mwanafunzi afanye maendeleo.
WAKATI: Hotuba na maelezo ya mshauri hayapaswi kamwe kupita wakati. Wanafunzi wanaotoa hotuba Na. 1, Na. 2, na Na. 3 wanapaswa kukatizwa kwa busara muda wao unapokwisha. Ndugu wanaotoa mambo makuu ya usomaji wa Biblia wakipita wakati, wanapaswa kushauriwa faraghani. Wote wanapaswa kufuata wakati. Programu nzima: Dakika 30.
FOMU YA MASHAURI: Imo katika kitabu Shule ya Huduma.
MSHAURI MSAIDIZI: Mbali na mwangalizi wa shule, baraza la wazee linaweza kuchagua mzee mwenye uwezo, ikiwa yupo, awe mshauri msaidizi. Ikiwa kuna wazee kadhaa kutanikoni, kila mwaka, mzee tofauti anayestahili anaweza kupewa mgawo huo. Mshauri msaidizi ana daraka la kuwashauri faraghani akina ndugu wanaotoa mambo makuu ya usomaji wa Biblia, inapohitajiwa. Hahitaji kuwashauri wazee wenzake au watumishi wa huduma kila mara wanapotoa hotuba hizo.
PITIO LA SHULE YA HUDUMA YA KITHEOKRASI: Dakika 20. Baada ya kila miezi miwili, mwangalizi wa shule ataongoza pitio. Sehemu hiyo itafanywa baada ya mambo makuu ya usomaji wa Biblia kama inavyoonyeshwa hapo juu. Pitio hilo litahusisha habari zilizozungumziwa katika shule miezi miwili iliyotangulia, kutia ndani juma la pitio. Ikiwa kutaniko lenu lina kusanyiko la mzunguko au ziara ya mwangalizi wa mzunguko wakati wa juma la Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi, basi pitio litafanywa juma litakalofuata, na Hotuba Na. 1, Na 2, na Na. 3 katika ratiba ya juma linalofuata zitatolewa katika kusanyiko hilo la mzunguko au wakati wa ziara ya mwangalizi wa mzunguko. Hakutakuwa na mabadiliko yoyote katika usomaji wa Biblia wa juma hilo na mambo makuu ya usomaji huo.
RATIBA
Jan. 5 Usomaji wa Biblia: Mwanzo 1-5
Na. 1: Mwanzo 3:1-15
Na. 2: Kwa Nini Yesu Alikuwa Mwalimu Mkuu? (lr sura ya 1)
Na. 3: Ni Jambo Gani Ambalo Si Ubatili? (1 Kor. 15:58)
Jan. 12 Usomaji wa Biblia: Mwanzo 6-10
Na. 1: Mwanzo 9:1-17
Na. 2: Kujibu Maswali ya Watu Wasiomwamini Mungu (rs uku. 220 ¶1–uku. 221 ¶2)
Na. 3: Barua Kutoka kwa Mungu Mwenye Upendo (lr sura ya 2)
Jan. 19 Usomaji wa Biblia: Mwanzo 11-16
Na. 1: Mwanzo 14:1-16
Na. 2: Ni Nani Aliyeviumba Vitu Vyote? (lr sura ya 3)
Na. 3: Yehova Anatufinyanga Jinsi Gani? (Isa. 64:8)
Jan. 26 Usomaji wa Biblia: Mwanzo 17-20
Na. 1: Mwanzo 17:1-17
Na. 2: Kwa Nini Wanadamu Wameshindwa Kuanzisha Serikali Yenye Haki? (rs uku. 265-266 ¶2)
Na. 3: Mungu Ana Jina (lr sura ya 4)
Feb. 2 Usomaji wa Biblia: Mwanzo 21-24
Na. 1: Mwanzo 22:1-18
Na. 2: “Huyu Ni Mwanangu” (lr sura ya 5)
Na. 3: a Jinsi ya Kupanua Upendo Wetu kwa Wengine (2 Kor. 6:11-13)
Feb. 9 Usomaji wa Biblia: Mwanzo 25-28
Na. 1: Mwanzo 25:1-18
Na. 2: Mwalimu Mkuu Aliwahudumia Wengine (lr sura ya 6)
Na. 3: Kwa Nini Jitihada za Wanadamu za Kuleta Kitulizo Haziwezi Kufanikiwa? (rs uku. 266 ¶3–uku. 267 ¶2)
Feb. 16 Usomaji wa Biblia: Mwanzo 29-31
Na. 1: Mwanzo 29:1-20
Na. 2: Kwa Nini ‘Tuache Kuhangaika’? (Mt. 6:25)
Na. 3: Utii Unakulinda Wewe (lr sura ya 7)
Feb. 23 Usomaji wa Biblia: Mwanzo 32-35
Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
Mac. 2 Usomaji wa Biblia: Mwanzo 36-39
Na. 1: Mwanzo 39:1-16
Na. 2: Wengine Wana Mamlaka Kuliko Sisi (lr sura ya 8)
Na. 3: Ufalme wa Mungu Ndio Suluhisho Pekee kwa Mahitaji Halisi ya Wanadamu (rs uku. 267 ¶3–uku. 268 ¶1)
Mac. 9 Usomaji wa Biblia: Mwanzo 40-42
Na. 1: Mwanzo 40:1-15
Na. 2: Tuepuke Vishawishi (lr sura ya 9)
Na. 3: b Jihadhari na Roho ya Kujitegemea!
Mac. 16 Usomaji wa Biblia: Mwanzo 43-46
Na. 1: Mwanzo 44:1-17
Na. 2: Yesu Ana Nguvu Kuliko Roho Waovu (lr sura ya 10)
Na. 3: Unabii wa Biblia Umekuwa Wenye Kutegemeka Kabisa (rs uku. 268 ¶2-uku. 269 ¶1)
Mac. 23 Usomaji wa Biblia: Mwanzo 47-50
Na. 1: Mwanzo 48:1-16
Na. 2: Je, Tumwogope Ibilisi?
Na. 3: Msaada wa Malaika wa Mungu (lr sura ya 11)
Mac. 30 Usomaji wa Biblia: Kutoka 1-6
Na. 1: Kutoka 1:1-19
Na. 2: Yesu Anatufundisha Kusali (lr sura ya 12)
Na. 3: Je, Uponyaji wa Kimuujiza Leo Unafanywa Kupitia Roho ya Mungu? (rs uku. 355-356 ¶2)
Apr. 6 Usomaji wa Biblia: Kutoka 7-10
Na. 1: Kutoka 9:1-19
Na. 2: Wale Walioitwa Wawe Wanafunzi wa Yesu (lr sura ya 13)
Na. 3: c Tunaweza Kupatanishaje Wagalatia 6:2 na Wagalatia 6:5?
Apr. 13 Usomaji wa Biblia: Kutoka 11-14
Na. 1: Kutoka 12:21-36
Na. 2: Kwa Nini Tuwe Wenye Kusamehe? (lr sura ya 14)
Na. 3: Tofauti Kati ya Maponyo Yaliyofanywa na Yesu na Mitume Wake na Yale Yanayofanywa Leo (rs uku. 356 ¶3–uku. 357 ¶2)
Apr. 20 Usomaji wa Biblia: Kutoka 15-18
Na. 1: Kutoka 15:1-19
Na. 2: Kuepuka Ibada ya Uwongo Kunahusisha Nini?
Na. 3: Jinsi ya Kuwa Mwenye Fadhili (lr sura ya 15)
Apr. 27 Usomaji wa Biblia: Kutoka 19-22
Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
Mei 4 Usomaji wa Biblia: Kutoka 23-26
Na. 1: Kutoka 24:1-18
Na. 2: Ni Nini Ambacho kwa Kweli Ni cha Maana Maishani? (lr sura ya 16)
Na. 3: Mambo Yanayowatambulisha Wakristo wa Kweli Leo (rs uku. 357 ¶3–uku. 358 ¶1)
Mei 11 Usomaji wa Biblia: Kutoka 27-29
Na. 1: Kutoka 29:1-18
Na. 2: Jinsi ya Kuwa Wenye Furaha (lr sura ya 17)
Na. 3: d Hatari za Ushikamanifu Usiofaa
Mei 18 Usomaji wa Biblia: Kutoka 30-33
Na. 1: Kutoka 31:1-18
Na. 2: Kwa Nini Wakristo wa Karne ya Kwanza Walipewa Zawadi za Kuponya? (rs uku. 358 ¶2–uku. 359 ¶2)
Na. 3: Je, Wewe Hukumbuka Kusema Asante? (lr sura ya 18)
Mei 25 Usomaji wa Biblia: Kutoka 34-37
Na. 1: Kutoka 37:1-24
Na. 2: Je, Ni Vizuri Kupigana? (lr sura ya 19)
Na. 3: e Uendekevu Ni Nini, na kwa Nini Tuuepuke?
Juni 1 Usomaji wa Biblia: Kutoka 38-40
Na. 1: Kutoka 40:1-19
Na. 2: Je, Unapenda Kujitanguliza Kila Wakati? (lr sura ya 20)
Na. 3: Kuna Tumaini Gani kwa Wanadamu Wote Kuponywa Kikweli? (rs uku. 359 ¶3-5)
Juni 8 Usomaji wa Biblia: Mambo ya Walawi 1-5
Na. 1: Mambo ya Walawi 4:1-15
Na. 2: Je, Ni Vizuri Kujisifia Jambo Lolote? (lr sura ya 21)
Na. 3: f Wakristo Wanapaswa Kutumiaje Mamlaka?
Juni 15 Usomaji wa Biblia: Mambo ya Walawi 6-9
Na. 1: Mambo ya Walawi 8:1-17
Na. 2: ‘Je, Unaamini Uponyaji?’ (rs uku. 359 ¶6–uku. 360 ¶1)
Na. 3: Kwa Nini Hatupaswi Kusema Uwongo? (lr sura ya 22)
Juni 22 Usomaji wa Biblia: Mambo ya Walawi 10-13
Na. 1: Mambo ya Walawi 11:29-45
Na. 2: Kwa Nini Tunakuwa Wagonjwa? (lr sura ya 23)
Na. 3: Baraka Ambazo Wanafunzi Waliobatizwa Hupata
Juni 29 Usomaji wa Biblia: Mambo ya Walawi 14-16
Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
Julai 6 Usomaji wa Biblia: Mambo ya Walawi 17-20
Na. 1: Mambo ya Walawi 19:1-18
Na. 2: Je, Sisi Sote Tulikuwa Katika Makao ya Kiroho Kabla Hatujazaliwa Tukiwa Wanadamu? (rs uku. 197 ¶2–uku. 198 ¶3)
Na. 3: Usiwe Mwizi Kamwe! (lr sura ya 24)
Julai 13 Usomaji wa Biblia: Mambo ya Walawi 21-24
Na. 1: Mambo ya Walawi 22:17-33
Na. 2: Je, Watu Wanaofanya Mabaya Wanaweza Kubadilika? (lr sura ya 25)
Na. 3: Jinsi Wakristo wa Kweli Wanavyowahangaikia Maskini
Julai 20 Usomaji wa Biblia: Mambo ya Walawi 25-27
Na. 1: Mambo ya Walawi 25:39-54
Na. 2: Kwa Nini Si Rahisi Kutenda Mema? (lr sura ya 26)
Na. 3: Kama Adamu Hangefanya Dhambi, je, Mwishowe Angeenda Mbinguni? (rs uku. 198 ¶4-5)
Julai 27 Usomaji wa Biblia: Hesabu 1-3
Na. 1: Hesabu 3:1-20
Na. 2: Kujizuia Kunahitajika Ili Tuwe Wapole
Na. 3: Mungu Wako Ni Nani? (lr sura ya 27)
Ago. 3 Usomaji wa Biblia: Hesabu 4-6
Na. 1: Hesabu 4:1-16
Na. 2: Jinsi ya Kujua Yule Tunayepaswa Kumtii (lr sura ya 28)
Na. 3: Je, Ni Lazima Mtu Aende Mbinguni Ndipo Awe na Maisha Yenye Furaha Kweli Kweli? (rs uku. 199 ¶1-3)
Ago. 10 Usomaji wa Biblia: Hesabu 7-9
Na. 1: Hesabu 9:1-14
Na. 2: Je, Karamu Zote Zinampendeza Mungu? (lr sura ya 29)
Na. 3: Jinsi Tunavyoweza Kumwonyesha Yehova Ushikamanifu
Ago. 17 Usomaji wa Biblia: Hesabu 10-13
Na. 1: Hesabu 13:17-33
Na. 2: Jinsi Tunavyoweza Kuushinda Woga (lr sura ya 30)
Na. 3: Andiko la 1 Petro 3:19, 20 Linamaanisha Nini? (rs uku. 199 ¶4)
Ago. 24 Usomaji wa Biblia: Hesabu 14-16
Na. 1: Hesabu 14:26-43
Na. 2: Kupenda Sheria ya Mungu Kunamaanisha Nini? (Zab. 119:97)
Na. 3: Mahali pa Kupata Faraja (lr sura ya 31)
Ago. 31 Usomaji wa Biblia: Hesabu 17-21
Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
Sept. 7 Usomaji wa Biblia: Hesabu 22-25
Na. 1: Hesabu 22:20-35
Na. 2: Jinsi Yesu Alivyolindwa (lr sura ya 32)
Na. 3: Andiko la 1 Petro 4:6 Linamaanisha Nini? (rs uku. 199 ¶5)
Sept. 14 Usomaji wa Biblia: Hesabu 26-29
Na. 1: Hesabu 27:1-14
Na. 2: Mwongozo wa Akilini Unamaanisha Nini, na Kwa Nini Ni Muhimu? (Efe. 6:4)
Na. 3: Yesu Anaweza Kutulinda (lr sura ya 33)
Sept. 21 Usomaji wa Biblia: Hesabu 30-32
Na. 1: Hesabu 32:1-15
Na. 2: Inakuwaje Tunapokufa? (lr sura ya 34)
Na. 3: Je, Wakristo Wote Wana Tumaini la Kuishi Mbinguni? (rs uku. 200 ¶1-3)
Sept. 28 Usomaji wa Biblia: Hesabu 33-36
Na. 1: Hesabu 33:1-23
Na. 2: Tunaweza Kufufuliwa! (lr sura ya 35)
Na. 3: Ufalme wa Mungu Ni Bora Kuliko Serikali za Wanadamu Kwa Njia Gani?
Okt. 5 Usomaji wa Biblia: Kumbukumbu la Torati 1-3
Na. 1: Kumbukumbu la Torati 2:1-15
Na. 2: “Agano Jipya” Husema Nini Kuhusu Uzima wa Milele Duniani? (rs uku. 201 ¶1–uku. 202 ¶2)
Na. 3: Ni Nani Watakaofufuliwa? Nao Wataishi Wapi? (lr sura ya 36)
Okt. 12 Usomaji wa Biblia: Kumbukumbu la Torati 4-6
Na. 1: Kumbukumbu la Torati 4:15-28
Na. 2: Kumkumbuka Yehova na Mwana Wake (lr sura ya 37)
Na. 3: Ni Wakati Gani Inaweza Kusemwa Kwamba Kuwa na Vitu Vichache Ni Bora? (Met. 15:16)
Okt. 19 Usomaji wa Biblia: Kumbukumbu la Torati 7-10
Na. 1: Kumbukumbu la Torati 9:1-14
Na. 2: Kwa Nini Tumpende Yesu? (lr sura ya 38)
Na. 3: Biblia Inawatolea Watu Wangapi Tumaini la Uzima wa Mbinguni? (rs uku. 202 ¶3-4)
Okt. 26 Usomaji wa Biblia: Kumbukumbu la Torati 11-13
Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
Nov. 2 Usomaji wa Biblia: Kumbukumbu la Torati 14-18
Na. 1: Kumbukumbu la Torati 15:1-15
Na. 2: Kumwogopa Mungu Kunahusisha Nini?
Na. 3: Mungu Amkumbuka Mwana Wake (lr sura ya 39)
Nov. 9 Usomaji wa Biblia: Kumbukumbu la Torati 19-22
Na. 1: Kumbukumbu la Torati 22:1-19
Na. 2: Jinsi ya Kumfurahisha Mungu (lr sura ya 40)
Na. 3: Je, Wale 144,000 Ni Wayahudi wa Asili Peke Yao? (rs uku. 202 ¶5–uku. 203 ¶3)
Nov. 16 Usomaji wa Biblia: Kumbukumbu la Torati 23-27
Na. 1: Kumbukumbu la Torati 25:1-16
Na. 2: Watoto Wanaomfurahisha Mungu (lr sura ya 41)
Na. 3: g Ni Mambo Gani Tunayopaswa Kuyaona Kuwa Matakatifu?
Nov. 23 Usomaji wa Biblia: Kumbukumbu la Torati 28-31
Na. 1: Kumbukumbu la Torati 30:1-14
Na. 2: Kwa Nini Tufanye Kazi? (lr sura ya 42)
Na. 3: Maandiko Husema Nini Kuhusu Tumaini la “Umati Mkubwa”? (rs uku. 203 ¶4–uku. 204 ¶1)
Nov. 30 Usomaji wa Biblia: Kumbukumbu la Torati 32-34
Na. 1: Kumbukumbu la Torati 32:1-21
Na. 2: “Ile Siku Kuu ya Yehova” Ni Nini? (Sef. 1:14)
Na. 3: Ndugu Zetu na Dada Zetu Ni Akina Nani? (lr sura ya 43)
Des. 7 Usomaji wa Biblia: Yoshua 1-5
Na. 1: Yoshua 5:1-15
Na. 2: Rafiki Zetu Wanapaswa Kuwa Watu Wanaompenda Mungu (lr sura ya 44)
Na. 3: Ufalme wa Mungu Ni Nini? Na Tunaonyeshaje Kwamba Tunautaka? (lr sura ya 45)
Des. 14 Usomaji wa Biblia: Yoshua 6-8
Na. 1: Yoshua 8:1-17
Na. 2: Je, Mungu Atauharibu Ulimwengu Tena Kwa Maji? (lr sura ya 46)
Na. 3: Kwa Nini Shauri la Mhubiri 7:21, 22 Linafaa?
Des. 21 Usomaji wa Biblia: Yoshua 9-11
Na. 1: Yoshua 9:1-15
Na. 2: Jinsi Tunavyoweza Kujua Har–Magedoni Imekaribia (lr sura ya 47)
Na. 3: Unaweza Kuishi Katika Ulimwengu Mpya wa Mungu Wenye Amani (lr sura ya 48)
Des. 28 Usomaji wa Biblia: Yoshua 12-15
Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
[Maelezo ya Chini]
a Hotuba hii itolewe na akina ndugu tu, ikiwezekana wazee au watumishi wa huduma.
b Hotuba hii itolewe na akina ndugu tu, ikiwezekana wazee au watumishi wa huduma.
c Hotuba hii itolewe na akina ndugu tu, ikiwezekana wazee au watumishi wa huduma.
d Hotuba hii itolewe na akina ndugu tu, ikiwezekana wazee au watumishi wa huduma.
e Hotuba hii itolewe na akina ndugu tu, ikiwezekana wazee au watumishi wa huduma.
f Hotuba hii itolewe na akina ndugu tu, ikiwezekana wazee au watumishi wa huduma.
g Hotuba hii itolewe na akina ndugu tu, ikiwezekana wazee au watumishi wa huduma.