Ratiba ya Juma Linaloanza Mei 10
JUMA LINALOANZA MEI 10
□ Funzo la Biblia la Kutaniko:
□ Shule ya Huduma ya Kitheokrasi:
Usomaji wa Biblia: 2 Samweli 4-8
Na. 1: 2 Samweli 6:1-13
Na. 2: Tunajua Nini Kuhusu Siku ya Wapendanao, Siku ya Mama, na Sikukuu za Taifa? (rs uku. 281 ¶4–uku. 282 ¶4)
Na. 3: Kwa Nini Pupa Ni Ibada ya Sanamu? (Efe. 5:5)
□ Mkutano wa Utumishi:
Dak. 5: Matangazo.
Dak. 10: Wape Watu Katika Eneo Msaada Unaofaa. Mazungumzo pamoja na wasikilizaji yanayotegemea kitabu Shule ya Huduma, ukurasa wa 188, fungu la 4, hadi mwisho wa ukurasa wa 189. Mhoji kifupi mhubiri ambaye alisaidiwa kufanya maendeleo kwa sababu wengine walionyesha kwamba wanamjali.
Dak. 10: Jumba Safi la Ufalme Humletea Yehova Sifa. Hotuba itolewe na mzee. Yehova ni Mungu safi, hivyo, watu wake wanapaswa kuzingatia sana usafi. (Kut. 30:17-21; 40:30-32) Tunapotunza na kuweka mahali petu pa ibada pakiwa safi, tunamletea Yehova utukufu. (1 Pet. 2:12) Mhoji ndugu anayesimamia usafi na utunzaji wa Jumba la Ufalme kuhusu mipango iliyopo ya kutunza jumba lenu. Simulia mambo yaliyoonwa katika eneo lenu au yale ambayo yamechapishwa, yanayoonyesha kwamba Jumba safi la Ufalme na lililotunzwa linatoa ushahidi katika ujirani. Watie moyo wote wasaidie kutunza na kudumisha usafi wa Jumba la Ufalme na pia uwanja.
Dak. 10: “Hii Habari Njema Itahubiriwa!” Mazungumzo kwa maswali na majibu.