Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 5/10 uku. 1
  • ‘Hii Habari Njema Itahubiriwa’!

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • ‘Hii Habari Njema Itahubiriwa’!
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2010
  • Habari Zinazolingana
  • Je, Unatimiza Huduma Yako Kikamili?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2019
  • Mwamuzi Mnyenyekevu Aliyetaka kuwa na Hakika
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
  • Kuendeleza Huduma Yetu Bila Kuacha
    Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • “Nendeni Mkafanye Wanafunzi Kutoka kwa Watu wa Mataifa Yote”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2016
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2010
km 5/10 uku. 1

‘Hii Habari Njema Itahubiriwa’!

1. Tunajuaje kwamba hakuna chochote kinachoweza kukomesha kazi ya kuhubiri?

1 Hakuna chochote kinachoweza kumzuia Yehova asitimize mapenzi yake. (Isa. 14:24) Ingawa ilionekana kuwa Mwamuzi Gideoni pamoja na wanaume wake 300 hawangeweza kushinda askari-jeshi Wamidiani wapatao 135,000, Yehova alimwambia hivi: “Hakika utawaokoa Israeli kutoka katika mkono wa Midiani. Je, si mimi ninayekutuma?” (Amu. 6:14) Ni kazi gani ambayo inategemezwa na Yehova leo? Yesu alisema: “Hii habari njema ya ufalme itahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa.” (Mt. 24:14) Hakuna mtu anayeweza kuikomesha kazi hii!

2. Kwa nini tunaweza kutarajia kwamba Yehova atamsaidia kila mmoja wetu katika huduma?

2 Yehova Anamsaidia Kila Mmoja Wetu: Ingawa tunajua Yehova atawafanikisha Mashahidi wake wakiwa kikundi, je, tunaweza kutarajia kwamba Yehova atatusaidia sisi binafsi? Alipokuwa na uhitaji, mtume Paulo alihisi kuwa Yehova alimsaidia kupitia Mwanaye, Yesu. (2 Tim. 4:17) Tunaweza kuwa na hakika kwamba Yehova atabariki pia jitihada za kila mmoja wetu za kufanya mapenzi yake.—1 Yoh. 5:14.

3. Yehova anatusaidia katika hali zipi mbalimbali?

3 Je, mahangaiko ya kila siku hufanya ukose nguvu za kuhubiri? “Yeye anampa nguvu mtu aliyechoka.” (Isa. 40:29-31) Je, unakabili mateso au upinzani? “Mtupie Yehova mzigo wako, naye mwenyewe atakutegemeza.” (Zab. 55:22) Je, nyakati nyingine unashikwa na woga wa kuhubiri? “Nenda, nami nitakuwa pamoja na kinywa chako.” (Kut. 4:11, 12) Je, matatizo ya afya yanakuzuia usifanye mengi katika utumishi? Yehova anathamini jitihada zako za moyo wote na anaweza kuzitumia, hata usipoweza kufanya mengi.—1 Kor. 3:6, 9.

4. Kuwa na hakika kwamba Yehova anabariki huduma yetu kutatuchochea tufanye nini?

4 Mkono wa Yehova “umenyooshwa, na ni nani anayeweza kuurudisha nyuma?” (Isa. 14:27) Kwa kuwa tuna hakika kwamba Yehova anabariki huduma yetu, acheni tuendelee kuhubiri “kwa ujasiri kwa mamlaka ya Yehova.”—Mdo. 14:3.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki