Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Aprili 1
“Maandishi fulani yanadai kwamba Yesu hakufa kama Biblia inavyosema bali alioa na kuzaa watoto. Je, umewahi kusikia jambo hili? [Mruhusu ajibu.] Ni muhimu kujua ukweli. [Soma Yohana 17:3.] Makala hii inatupatia sababu za kuamini masimulizi ya Biblia kumhusu Yesu.” Mwonyeshe makala inayoanzia ukurasa wa 26.
Amkeni! Aprili
Soma Zaburi 37:9-11, kisha uulize: “Unafikiri hali zitakuwaje duniani wakati unabii huu utakapotimia? [Mruhusu ajibu.] Makala hii inarejelea unabii huo unaotia moyo na inaeleza kwa nini kuna uovu mwingi sana duniani leo.” Mwonyeshe makala inayoanzia ukurasa wa 20.
Mnara wa Mlinzi Mei 1
“Je, umewahi kujiuliza kwa nini Mungu anawaacha watu wateseke? [Mruhusu ajibu.] Swali hili ambalo watu wengi wameuliza lilimhangaisha pia mwandikaji mmoja wa Biblia. [Soma Zaburi 10:1.] Gazeti hili linaonyesha maoni ya Biblia kuhusu kwa nini Mungu anawaacha watu wateseke na jinsi ambavyo ataleta kitulizo.”
Amkeni! Mei
“Watu wengi wanaovuta sigara wanataka kuacha zoea hili, lakini wameshindwa. Je, unamjua yeyote anayetaka kuacha kuvuta sigara? [Mruhusu ajibu.] Watu fulani wamenufaika kwa kuwaomba marafiki na watu wa familia wawasaidie. [Soma Mhubiri 4:12a.] Gazeti hili lina mapendekezo kadhaa yanayoweza kumsaidia mtu aache kuvuta sigara.”