Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 10/10 uku. 2
  • Broshua Mpya Tutakayotoa!

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Broshua Mpya Tutakayotoa!
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2010
  • Habari Zinazolingana
  • Jinsi ya Kutumia Broshua Habari Njema Kutoka kwa Mungu!
    Huduma ya Ufalme—2013
  • Mwige Yehova kwa Kujali Wengine Kikweli
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Je, Unazitumia Broshua Hizi?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2012
  • Tangaza Habari Njema za Ufalme Ukitumia Broshua
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2010
km 10/10 uku. 2

Broshua Mpya Tutakayotoa!

1. Tutatoa broshua gani mwezi wa Novemba, na kusudi la broshua hiyo ni nini?

1 Katika Kusanyiko la Wilaya la “Endeleeni Kukesha!” la 2009, broshua mpya yenye kichwa Biblia—Ina Ujumbe Gani? ilitolewa. Katika mwezi wa Novemba, makutaniko ulimwenguni pote yatatoa broshua hiyo kwa mara ya kwanza katika utumishi wa shambani. Broshua hiyo itawasaidiaje watu katika eneo letu? Watu wengi, hasa wale ambao si wa dini za Kikristo, hawajui mengi kuhusu Biblia. Hivyo, katika ukurasa wa 3, broshua hiyo inaeleza kwamba imekusudiwa kuwasaidia watu kupata “picha ya ujumla kuhusu Biblia.”

2. Tunaweza kutoaje broshua hiyo?

2 Jinsi ya Kuitoa: Tunaweza kusema hivi: “Tungependa kupata maoni yako kuhusu andiko hili. [Soma 2 Timotheo 3:16.] Watu wengi tunaozungumza nao hukubaliana na maneno haya; wengine huhisi kwamba Biblia ni kitabu kizuri tu. Una maoni gani kuhusu Biblia? [Mruhusu ajibu.] Haidhuru mambo tunayoamini, kuna sababu nzuri za kuichunguza Biblia sisi wenyewe. [Soma fungu la utangulizi katika sehemu ya juu ya ukurasa wa 3.] Unaposoma muhtasari wenye kusisimua wa Biblia unaopatikana katika broshua hii, utatambua jambo fulani lenye kupendeza: Biblia ina habari moja kuu.”

3. Tunaweza kutumia njia gani nyingine kutoa broshua hiyo, hasa katika eneo ambalo wengi ni wa dini zisizo za Kikristo?

3 Ama tunaweza kusema hivi, hasa tunapohubiri katika eneo ambalo watu wengi si wa dini za Kikristo: “Tungependa kupata maoni yako kuhusu habari hii tunayosoma katika Maandiko (au katika kitabu hiki kitakatifu). [Soma Zaburi 37:11.] Unafikiri dunia itakuwaje unabii huu utakapotimizwa? [Mruhusu ajibu.] Huu ni mfano wa tumaini na faraja ambazo watu wa tamaduni na imani zote wanaweza kupata katika Biblia.” Soma fungu lililo katika sehemu ya juu ya ukurasa wa 3, kisha umpe broshua.

4. Tunaweza kutumia broshua hiyo jinsi gani kuanzisha funzo la Biblia?

4 Anzisha Funzo la Biblia: Tunapomrudia mwenye nyumba tunaweza kumkumbusha mambo tuliyozungumzia wakati uliopita na tuzungumzie fungu moja au mawili kuhusu habari tulizozungumzia, tukitumia maswali yaliyo mwishoni mwa sehemu tuliyochagua. Au tukipenda kutoa kitabu Biblia Inafundisha wakati huo, tunaweza kusoma pamoja na mtu huyo ukurasa wa nyuma wa broshua hiyo, tumpe kitabu, tumuulize ni sura gani inayompendeza, kisha tuchunguze pamoja fungu moja au mawili katika sura hiyo. Acheni sote tushiriki kikamili katika kutoa broshua hiyo mwezi wa Novemba!

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki