Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Novemba 1
“Unafikiri malaika wanapendezwa na mambo tunayofanya? [Mruhusu ajibu.] Biblia inatoa taarifa hii yenye kupendeza. [Soma Luka 15:10.] Makala hii inazungumzia mambo ambayo Yesu alisema kuhusu jinsi viumbe wa roho wanavyoweza kuwa na uvutano katika maisha yetu.” Mwonyeshe makala inayoanzia ukurasa wa 16.
Amkeni! Novemba
Soma 2 Timotheo 3:16. Kisha useme: “Unakubali na kuamini kwamba tunaweza kutumaini kila jambo ambalo Biblia inasema? [Mruhusu ajibu.] Makala hii inaonyesha ikiwa historia na vitu vya kale vilivyochimbuliwa zinaunga mkono mambo ambayo Biblia inasema kuhusu Misri ya kale.” Mwonyeshe makala inayoanzia ukurasa wa 15.
Mnara wa Mlinzi Desemba 1
“Watu wengi wanaamini kwamba kuna viumbe wenye akili walio katika makao ya roho ambao wana uvutano katika maisha yetu. Una maoni gani? [Mruhusu ajibu, kisha usome Ufunuo 12:7-9.] Gazeti hili linaonyesha mambo ambayo Biblia inasema kuhusu wale wanaoishi katika makao ya roho, uvutano walio nao juu yetu, na kama tunaweza kuwasiliana nao.”
Amkeni! Desemba
“Umewahi kujiuliza ni kwa nini watu husherehekea Krismasi tarehe 25 mwezi wa Desemba ilhali Biblia haitaji wakati ambapo Yesu alizaliwa? [Mruhusu ajibu.] Kulingana na mstari huu, haiwezekani kwamba Yesu alizaliwa wakati wa majira ya baridi kali. [Soma Luka 2:8.] Gazeti hili linazungumzia chanzo cha baadhi ya desturi zinazopendwa za Krismasi.”