Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Desemba 1
“Mwezi huu wa Desemba, watu wengi hutayarisha mandhari inayoonyesha mazingira ambamo Yesu alizaliwa, ambayo yanaelezwa katika andiko hili la Biblia. [Soma Mathayo 2:1, 11.] Je, umeona tofauti kati ya yale ambayo Biblia inasema yalitukia na mambo ambayo kwa kawaida huonyeshwa katika mandhari hizo? [Mruhusu ajibu.] Makala hii inazungumzia mambo yaliyotukia.” Mwonyeshe makala kwenye ukurasa wa 31.
Amkeni! Desemba
“Ningependa kujua maoni yako kuhusu jambo fulani ambalo Yesu alisema. [Soma Mathayo 5:3.] Kwa kuwa kuna dini nyingi tofauti-tofauti, je, unafikiri ni muhimu kuchunguza jinsi tunavyotosheleza uhitaji wetu wa kiroho? [Mruhusu ajibu.] Makala hii inaonyesha yale ambayo Biblia inasema kuhusu jinsi ya kupata uradhi wa kweli wa kiroho.” Mwonyeshe makala inayoanzia ukurasa wa 12.
Mnara wa Mlinzi Januari 1
“Dini zina maoni yanayotofautiana kuhusu pombe. Unafikiri Mungu anamwonaje mtu anayekunywa pombe? [Mruhusu ajibu.] Ingawa Biblia inasema kwamba pindi moja Yesu alibadili maji kimuujiza yakawa divai, pia inasema hivi. [Soma Methali 23:20a.] Gazeti hili linaonyesha maoni ya Biblia yenye usawaziko.”
Amkeni! Januari
“Katika nyakati hizi ngumu, watu wengi huhisi kwamba wanafanya kazi kupita kiasi na wamechoka. Je, umewahi kuhisi hivyo? [Mruhusu ajibu.] Ona ushauri huu mzuri. [Soma Mhubiri 4:6.] Gazeti hili linazungumzia jinsi tunavyoweza kuwa wenye usawaziko kuhusiana na kazi, familia, na burudani. Pia linatoa madokezo kwa wale wanaotafuta kazi.”