Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Desemba 1
“Je, unakubaliana nami kwamba wazazi wasio na wenzi wa ndoa wana majukumu mengi kuliko wale walio na wenzi wa ndoa? [Mruhusu ajibu.] Biblia inatutia moyo tuwajali watu wanaokabiliana na matatizo mbalimbali. [Soma Zaburi 41:1.] Makala inayoanzia ukurasa wa 22 inaonyesha jinsi tunavyoweza kuwajali wazazi wasio na wenzi wa ndoa.”
Amkeni! Desemba
“Watu wengi huuliza, ‘Ikiwa kuna Mungu, kwa nini hajamwangamiza Ibilisi?’ Umewahi kujiuliza swali hilo? [Mruhusu ajibu.] Makala hii katika ukurasa wa 10 na 11 inajibu swali hilo kutoka katika Biblia. Pia, inaonyesha jinsi ulimwengu utakavyokuwa baada ya Ibilisi kuondolewa.” Soma Ufunuo 21:3, 4.
Mnara wa Mlinzi Januari 1
“Watu wengi wanaamini kwamba masimulizi kuhusu bustani ya Edeni ni ya kubuniwa tu. Je, ungeshangaa kujua kwamba Yesu aliwataja Adamu na Hawa kuwa watu halisi? [Mruhusu ajibu, kisha usome Mathayo 19:4-6.] Gazeti hili linajibu maswali fulani ambayo watu wengi huuliza kuhusu bustani ya Edeni.”
Amkeni! Januari
Mwonyeshe gazeti na umuulize, “Ungejibuje swali hili? [Mruhusu ajibu.] Maandiko huwatia moyo watu wawe wenye kufanya amani. [Soma Yakobo 3:17.] Hivyo basi, kwa nini dini haijawaunganisha wanadamu? Je, dini itawahi kuwachochea watu wawe wenye amani? Gazeti hili linachunguza majibu ya maswali hayo.”