Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi
Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Katika Jumamosi ya Kwanza Mwezi wa Mei
“Je, umewahi kujiuliza kwa nini Mungu anaruhusu uovu na kuteseka? [Mruhusu ajibu.] Ningependa kukuonyesha jambo fulani linalopendeza kuhusu jambo hilo.” Someni pamoja habari zilizo chini ya kichwa kidogo cha kwanza katika ukurasa wa 16 wa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Mei 1, na mojawapo ya maandiko yaliyoonyeshwa. Mtolee magazeti na upange kurudi ili mchunguze jibu la swali linalofuata.
Mnara wa Mlinzi Mei 1
Soma Zaburi 37:10, 11, kisha useme: “Unafikiri tutaona ahadi hii ikitimizwa hivi karibuni? [Mruhusu ajibu.] Gazeti hili linazungumzia mambo sita yaliyotabiriwa katika Biblia, na ambayo tunaona yakitimia sasa. Mambo hayo yanaonyesha kwamba ahadi hiyo katika kitabu cha Zaburi itatimizwa hivi karibuni.”
Amkeni! Mei
“Watu wengi husema kuwa wanadamu ni wanyama tu lakini ambao ni wa hali ya juu kuliko wanyama wengine. Wewe una maoni gani? [Mruhusu ajibu, kisha usome Zaburi 139:14.] Ijapokuwa mtunga-zaburi alisema maneno hayo, hakufahamu kabisa jinsi mwili wa mwanadamu ulivyoumbwa. Gazeti hili linazungumzia mambo ambayo tunayafahamu sasa, kutia ndani mambo yanayotutofautisha na wanyama.”