Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi
Kuanzisha mafunzo ya Biblia katika Jumamosi ya kwanza mwezi wa Agosti
“Kuna dini nyingi na watu humwabudu Mungu kupitia njia nyingi mbalimbali. Unafikiri Mungu anaonaje jambo hilo? [Mruhusu ajibu.] Ona kile ambacho Yesu alifundisha kuhusiana na hilo.” Mpe mwenye nyumba nakala ya Mnara wa Mlinzi wa Agosti 1. Pitieni habari zilizo chini ya kichwa kidogo cha kwanza katika ukurasa wa 16 na angalau moja ya maandiko yaliyotajwa. Mtolee magazeti, na upange kurudi ili mchunguze jibu la swali linalofuata.
Mnara wa Mlinzi Agosti 1
“Je, watoto wanapaswa kufundishwa kumhusu Mungu wakiwa wachanga au ni vyema zaidi kungoja mpaka watakapokuwa wakubwa ili wajichagulie wenyewe mambo ya kidini watakayoamini? [Mruhusu ajibu.] Ona kile ambacho Biblia inawaagiza kina baba wafanye. [Soma Waefeso 6:4.] Gazeti hili lina madokezo ya jinsi wazazi wanavyoweza kuwafundisha watoto wao kumhusu Mungu.”
Amkeni! Agosti
“Ningependa kusikia maoni yako kuhusu andiko hili. [Soma 1 Samweli 16:23.] Kulingana na andiko hilo, muziki una nguvu. Je, unafikiri inawezekana nyimbo fulani kuwa na uvutano mbaya? [Mruhusu ajibu.] Gazeti hili linazungumzia jinsi tunavyoweza kuchagua kwa hekima aina ya muziki tunaosikiliza, na jinsi tunavyoweza kuwasaidia watoto wetu kufanya hivyo pia.”