Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi
Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Katika Jumamosi ya Kwanza Mwezi wa Agosti
“Karibu kila mtu husali wakati fulani. Hata wale wasioamini kwamba kuna Mungu husali wanapopatwa na matatizo. Je, unafikiri Mungu husikiliza sala zote?” Mruhusu ajibu. Mwonyeshe ukurasa wa nyuma wa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Agosti 1 na mzungumzie habari iliyo chini ya swali la kwanza na angalau mojawapo ya maandiko yaliyoonyeshwa. Mwachie magazeti na ufanye mipango ya kurudi ili mzungumzie swali linalofuata.
Zingatia: Kwa kutumia pendekezo lililo hapo juu, fanyeni mpango kuwe na onyesho litakalofanywa tarehe 3 mwezi wa Agosti wakati wa mkutano wa utumishi wa shambani.
Mnara wa Mlinzi Agosti 1
“Tunawatembelea kwa muda mfupi kwa sababu watu wengi wanashtushwa na jinsi ambavyo ponografia imeenea kwa kiwango kikubwa. Hata hivyo, wengine wengi huhisi kwamba ponografia haina madhara yoyote. Una maoni gani? [Mruhusu ajibu.] Yesu alisema kwamba tunaweza kutambua ikiwa jambo fulani ni zuri kutokana na matunda yake. [Soma Mathayo 7:17.] Gazeti hili linazungumzia matokeo ya ponografia. Pia, linatoa mapendekezo yanayofaa ya jinsi tunavyoweza kuacha zoea hilo.”
Amkeni! Agosti
“Wengi miongoni mwetu tungependa kuishi muda mrefu kadiri tuwezavyo. Je, unafikiri siku moja maendeleo ya kisayansi yatatuwezesha tuishi milele? [Mruhusu ajibu.] Ona ahadi hii inayosisimua. [Soma 1 Wakorintho 15:26.] Lakini Mungu atatimizaje jambo hilo? Je, ni kupitia sayansi au kupitia njia nyinginezo? Na kwa nini leo tunazeeka na kufa? Gazeti hili linaonyesha jinsi Biblia inavyojibu maswali hayo.”