Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 7/13 uku. 8
  • Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi
  • Huduma ya Ufalme—2013
  • Habari Zinazolingana
  • Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Ninaweza kuepukaje Ponografia?
    Amkeni!—2007
  • Kwa Nini Niepuke Ponografia?
    Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi, Buku la 2
  • Ponografia—Je, Ina Madhara?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
Pata Habari Zaidi
Huduma ya Ufalme—2013
km 7/13 uku. 8

Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi

Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Katika Jumamosi ya Kwanza Mwezi wa Agosti

“Karibu kila mtu husali wakati fulani. Hata wale wasioamini kwamba kuna Mungu husali wanapopatwa na matatizo. Je, unafikiri Mungu husikiliza sala zote?” Mruhusu ajibu. Mwonyeshe ukurasa wa nyuma wa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Agosti 1 na mzungumzie habari iliyo chini ya swali la kwanza na angalau mojawapo ya maandiko yaliyoonyeshwa. Mwachie magazeti na ufanye mipango ya kurudi ili mzungumzie swali linalofuata.

Zingatia: Kwa kutumia pendekezo lililo hapo juu, fanyeni mpango kuwe na onyesho litakalofanywa tarehe 3 mwezi wa Agosti wakati wa mkutano wa utumishi wa shambani.

Mnara wa Mlinzi Agosti 1

“Tunawatembelea kwa muda mfupi kwa sababu watu wengi wanashtushwa na jinsi ambavyo ponografia imeenea kwa kiwango kikubwa. Hata hivyo, wengine wengi huhisi kwamba ponografia haina madhara yoyote. Una maoni gani? [Mruhusu ajibu.] Yesu alisema kwamba tunaweza kutambua ikiwa jambo fulani ni zuri kutokana na matunda yake. [Soma Mathayo 7:17.] Gazeti hili linazungumzia matokeo ya ponografia. Pia, linatoa mapendekezo yanayofaa ya jinsi tunavyoweza kuacha zoea hilo.”

Amkeni! Agosti

“Wengi miongoni mwetu tungependa kuishi muda mrefu kadiri tuwezavyo. Je, unafikiri siku moja maendeleo ya kisayansi yatatuwezesha tuishi milele? [Mruhusu ajibu.] Ona ahadi hii inayosisimua. [Soma 1 Wakorintho 15:26.] Lakini Mungu atatimizaje jambo hilo? Je, ni kupitia sayansi au kupitia njia nyinginezo? Na kwa nini leo tunazeeka na kufa? Gazeti hili linaonyesha jinsi Biblia inavyojibu maswali hayo.”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki