Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 10/11 uku. 1
  • Msaidie Mwenye Nyumba Kufikiri

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Msaidie Mwenye Nyumba Kufikiri
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Habari Zinazolingana
  • Tumia Kitabu Kutoa Sababu Kwenye Ziara za Kurudia
    Huduma Yetu ya Ufalme—1992
  • Ziara za Kurudia Sahili na Zenye Matokeo
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
  • Tumia Ile Kanuni Bora Katika Huduma Yako
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Je! Wewe Unatumia Utangulizi Unaofaa?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1988
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2011
km 10/11 uku. 1

Msaidie Mwenye Nyumba Kufikiri

1. Ni njia gani ya kuhubiri iliyo yenye matokeo zaidi?

1 Ni njia gani ya kuhubiri iliyo yenye matokeo zaidi—kuhubiri kishupavu au kuhubiri kwa njia ambayo inamsaidia mwenye nyumba kufikiri na kufikia uamuzi unaofaa? Mtume Paulo alitumia njia hiyo ya pili alipokuwa akizungumza na Wayahudi huko Thesalonike, na kwa sababu hiyo “baadhi yao wakawa waamini.” (Mdo. 17:2-4) Kuwasaidia watu kufikiri kunahusisha nini?

2. Tunaweza kuigaje mfano wa Paulo tunapohubiri habari njema?

2 Fikiria Hisia na Malezi: Ili kuwasaidia watu katika eneo kufikiri, ni lazima ufikirie hisia zao. Paulo alianza hotuba aliyowatolea Wagiriki wasioamini katika Areopago kwa kutaja mambo ambayo yaelekea waliyajua na kuyakubali. (Mdo. 17:22-31) Kwa hiyo, unapotayarisha utoaji wako, fikiria maoni na itikadi za watu katika eneo lenu. (1 Kor. 9:19-22) Mwenye nyumba akitokeza upinzani, jaribu kutafuta jambo ambalo nyote mnakubaliana, na ulitumie kama msingi wa mazungumzo yako.

3. Tunaweza kuwa wenye matokeo zaidi jinsi gani tunapojadiliana na wengine kwa kutumia maswali kwa ustadi?

3 Tumia Maswali kwa Ustadi: Hatuwezi kumpa msafiri mwongozo utakaomsaidia kufika anakoenda iwapo hatujui mahali alipo kwa sasa. Vivyo hivyo, hatuwezi kumsaidia mwenye nyumba kufanya uamuzi unaofaa iwapo hatujui maoni yake ya sasa. Kabla ya kuzungumza na msikilizaji, mara nyingi Yesu aliuliza maswali ili kujua maoni ya mtu huyo. Kwa mfano, mtu fulani alipomuuliza Yesu, “Nifanye nini ili niurithi uzima wa milele?,” Yesu alitaka kujua maoni ya mtu huyo kabla ya kumjibu. (Luka 10:25-28) Katika pindi nyingine, Petro alipotoa jibu lisilo sahihi, kwa ustadi Yesu alitumia maswali kurekebisha kufikiri kwa Petro. (Mt. 17:24-26) Kwa hiyo, ikiwa mwenye nyumba anauliza swali au anatoa maoni yasiyo sahihi, tunaweza kutumia maswali ili kumsaidia kufikiri.

4. Kwa nini tujaribu kumsaidia mwenye nyumba kufikiri?

4 Tunapomsaidia mwenye nyumba kufikiri, tunamwiga Mwalimu Mkuu Yesu, na pia waeneza-injili wengine wenye ustadi wa karne ya kwanza. Tunamwonyesha mwenye nyumba heshima na staha. (1 Pet. 3:15) Kwa kufanya hivyo, huenda akaturuhusu tumrudie.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki