Mabadiliko Katika Mkutano wa Katikati ya Juma
Kuanzia juma la Septemba 3, muda wa Funzo la Biblia la Kutaniko utaongezwa kutoka dakika 25 hadi 30. Katika maelezo yake ya utangulizi, ndugu anayeongoza anapaswa kutumia dakika moja kupitia habari za funzo lililotangulia. Pia, muda wa Mkutano wa Utumishi utabadilishwa kutoka dakika 35 hadi 30. Hakutakuwa tena na sehemu ya matangazo. Badala yake, ikiwa kuna matangazo yoyote, yanapaswa kutolewa mwanzoni mwa sehemu ya kwanza ya Mkutano wa Utumishi. Mara chache, ikihitajika, matangazo yanaweza kutolewa, hata hivyo hakuna haja ya kutangaza sehemu zitakazozungumziwa katika mkutano huo. Matangazo kuhusu mipango ya utumishi wa shambani, ratiba za usafi, na vilevile salamu hayapaswi kutolewa. (km 10/08 uku. 1, fu. 4) Ikiwa kutakuwa na tangazo refu, itakuwa vizuri ndugu walio na sehemu katika mkutano huo wajulishwe mapema ili wazifupishe.