Ratiba ya Juma Linaloanza Januari 7
JUMA LINALOANZA JANUARI 7, 2013
Wimbo 104 na Sala
□ Funzo la Biblia la Kutaniko:
jr sura ya 3 ¶13-19 (Dak. 30)
□ Shule ya Huduma ya Kitheokrasi:
Usomaji wa Biblia: Mathayo 1-6 (Dak. 10)
Na. 1: Mathayo 5:21-32 (Isizidi dak. 4)
Na. 2: Ni Nini Kinachoweza Kumfanya Mungu Asikubali Sala za Mtu?—rs uku. 258 ¶4–uku. 259 ¶2 (Dak. 5)
Na. 3: Kinachomaanishwa na Kumfanya Yehova Kuwa “Fungu Lako”—Hes. 18:20 (Dak. 5)
□ Mkutano wa Utumishi:
Dak. 10: Njia za Kutoa Magazeti Mwezi wa Januari. Mazungumzo. Tumia sekunde 30 hadi 60 kueleza kwa nini magazeti hayo yatawavutia watu katika eneo lenu. Kisha, kwa kutumia kichwa kilicho kwenye jalada la Mnara wa Mlinzi, waombe wasikilizaji wapendekeze swali linaloamsha upendezi watakalouliza na pia andiko ambalo watasoma. Fanya vivyo hivyo kuhusu gazeti la Amkeni! na, ikiwa wakati unaruhusu, zungumzia makala nyingine moja kutoka katika mojawapo ya magazeti hayo. Panga onyesho la jinsi kila gazeti linavyoweza kutolewa kwa kutumia magazeti ya karibuni zaidi mliyo nayo kutanikoni.
Dak. 10: Mahitaji ya kutaniko.
Dak. 10: Jumba Safi la Ufalme Humletea Yehova Heshima. Hotuba itolewe na mzee. Yehova ni Mungu mtakatifu, hivyo watu wake wanapaswa kuzingatia sana usafi. (Kut. 30:17-21; 40:30-32) Tunapotunza na kuweka mahali petu pa ibada pakiwa safi, tunamletea Yehova utukufu. (1 Pet. 2:12) Simulia mambo yaliyoonwa katika eneo lenu au kutoka katika machapisho yetu, yanayoonyesha jinsi Jumba safi la Ufalme lilivyotoa ushahidi katika ujirani. Mhoji ndugu anayesimamia usafi na udumishaji wa Jumba la Ufalme aeleze mipango iliyopo ya kutunza jumba lenu. Watie moyo wote wasaidie kusafisha na kudumisha Jumba la Ufalme.
Wimbo 127 na Sala