Ratiba ya Juma Linaloanza Februari 18
JUMA LINALOANZA FEBRUARI 18
Wimbo 52 na Sala
□ Funzo la Biblia la Kutaniko:
jr sura ya 5 ¶13-18 (Dak. 30)
□ Shule ya Huduma ya Kitheokrasi:
Usomaji wa Biblia: Marko 1-4 (Dak. 10)
Na. 1: Marko 2:18–3:6 (Isizidi dak. 4)
Na. 2: Msingi wa Fundisho la Toharani Ni Nini?—rs uku. 302 ¶1-uku. 303 ¶3 (Dak. 5)
Na. 3: Tunapaswa Kulielewaje Shauri la Paulo Linalopatikana Kwenye 1 Wakorintho 7:29-31? (Dak. 5)
□ Mkutano wa Utumishi:
Dak. 15: Lihubiri Neno Katika Majira Yenye Taabu. (2 Tim. 4:2) Mazungumzo yanayotegemea Kitabu cha Mwaka—2012, ukurasa wa 72, fungu la 1-2; ukurasa wa 110; ukurasa wa 156, fungu la 1, hadi ukurasa wa 157, fungu la 1; na ukurasa wa 179, fungu la 4. Waombe wasikilizaji watoe maelezo kuhusu masomo waliyojifunza.
Dak. 15: “Kampeni ya Kuwaalika Watu Kwenye Ukumbusho Itaanza Machi 1.” Maswali na majibu. Mpe kila mmoja aliyehudhuria nakala ya mwaliko, na uzungumzie yaliyomo katika mwaliko huo. Unapozungumzia fungu la 2, mwombe mwangalizi wa utumishi ataje mipango ya kutaniko lenu ya kuwafikia wengi iwezekanavyo katika eneo. Tumia pendekezo lililo kwenye ukurasa wa 4 kupanga onyesho la jinsi mwaliko huo unavyoweza kutolewa. Onyesho hilo lifanywe unapozungumzia fungu la 3.
Wimbo 8 na Sala