Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 10/13 uku. 2
  • Tumia Tovuti Yetu Kuwafundisha Watoto Wako

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Tumia Tovuti Yetu Kuwafundisha Watoto Wako
  • Huduma ya Ufalme—2013
  • Habari Zinazolingana
  • Tumia Tovuti ya jw.org/sw Katika Huduma—“Uwe Rafiki ya Yehova”
    Huduma Yetu ya Ufalme—2015
  • Jinsi Familia Yako Inavyoweza Kuwa na Furaha​—Sehemu ya 2
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
  • Tovuti ya Kipekee
    Amkeni!—2014
  • Dokezo la Kujifunza
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2023
Pata Habari Zaidi
Huduma ya Ufalme—2013
km 10/13 uku. 2

Tumia Tovuti Yetu Kuwafundisha Watoto Wako

1. Lengo la sehemu yenye kichwa “Watoto” katika Tovuti yetu ni nini?

1 Tovuti yetu ya jw.org, imekusudiwa kuwavutia watu wa umri mbalimbali. Katika Tovuti hiyo sehemu yenye kichwa “Watoto” (Mafundishao ya Biblia > Children)nenda kwa Mafundisho ya Biblia > Watoto) inawasaidia watoto kuwa na uhusiano wa karibu sana na wazazi wao na pia Yehova. (Kum. 6:6, 7) Unaweza kutumiaje sehemu hii kuwafundisha watoto wako?

2. Unawezaje kuchagua habari itakayowafaa watoto wako kulingana na umri wao?

2 Badilika Kulingana na Hali: Kila mtoto ana mahitaji yake ya pekee. (1 Kor. 13:11) Hivyo basi, unawezaje kuchagua habari itakayowafaa watoto wako kulingana na umri wao? Jiulize: ‘Ni mambo gani yatakayowafurahisha watoto wangu? Ni kiasi gani cha habari wanachoweza kuelewa? Wanaweza kumakinika kwa muda mrefu kadiri gani?’ Mnaweza kuzungumzia sehemu yenye kichwa .“Masomo Yangu ya Biblia” pamoja na watoto wenye umri wa miaka mitatu au walio chini ya umri huo.Masomo yangu ya Biblia.Familia nyingine hufurahia hadithi za Biblia zinazopatikana kwenye sehemu yenye kichwa “Wafundishe Watoto Wako.” Pia, fikiria mambo yafuatayo mnayoweza kufanya.

3. Wazazi wanaweza kutumiaje kikamilifu hadithi na mazoezi yanayopatikana kwenye sehemu ya “Miradi ya Ibada ya Familia”?

3 Miradi ya Ibada ya Familia: Miradi hii inaweza kuwasaidia wazazi wajifunze na watoto wao. Ili ujifunze jinsi ya kutumia sehemu ya hadithi na mazoezi, bonyeza kitufe cha kupakua na usome “Mwongozo kwa Wazazi” katika kila mradi. Tumia mazoezi ya picha kama vile ukurasa wa kupaka rangi unapowafundisha watoto wachanga. Wasaidie watoto wakubwa wajaze mazoezi ya kujifunza. Kila mradi una mazoezi mbalimbali na mazoezi yote hayo yanazungumzia hadithi na somo lilelile la Biblia. Jambo hilo linafanya watoto wa umri wowote ule waweze kushiriki katika mradi mmoja wa ibada ya familia.

4. Ni mambo gani yanayopatikana kwenye sehemu ya “Uwe Rafiki ya Yehova”?

4 Uwe Rafiki ya Yehova: Video, nyimbo, na mazoezi mbalimbali kwenye sehemu hii ya Tovuti yetu yanawasaidia wazazi wakazie Neno la Mungu mioyoni mwa watoto wao. (Kum. 31:12) Kila moja ya video hizo fupi za vibonzo inafundisha somo fulani muhimu. Kuna mazoezi ya kutafuta na kupata vitu ambayo yanakazia masomo hayo. Kwa kuwa watoto wanapenda kuimba na nyimbo zinawasaidia kukumbuka mambo waliyojifunza, Tovuti yetu huwa na nyimbo zetu za Ufalme na nyingine ambazo zimetungwa kwa ajili yao.

5.Ni kwa nini inafaa wazazi wamwombe Yehova awasaidie kuwafundisha watoto wao kweli?

5 Enyi wazazi, Yehova anataka mfanikiwe kuwalea watoto wenu. Kwa hiyo mwombeni awasaidie kuwafundisha watoto wenu kweli. (Amu. 13:8) Kwa msaada wa Yehova, unaweza kuwazoeza watoto wako ‘wawe wenye hekima kwa ajili ya wokovu kupitia imani kuhusiana na Kristo Yesu.’​—2 Tim. 3:15; Met. 4:1-4.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki