Ratiba ya Juma Linaloanza Oktoba 28
JUMA LINALOANZA OKTOBA 28
Wimbo 31 na Sala
□Funzo la Biblia la Kutaniko:
jl uku. 3 na Somo la 1-2 (Dak. 30)
□Shule ya Huduma ya Kitheokrasi:
Usomaji wa Biblia: 1 Timotheo 1–2 Timotheo 4 (Dak. 10)
Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokras (Dak. 20)
□Mkutano wa Utumishi:
Dak. 5:“Utafanya Nini Wakati wa Sikukuu?” Hotuba.
Dak.10:Kazia Faida za Habari Njema. Mazungumzo yanayotegemea kitabu Shule ya Huduma, ukurasa wa 159. Panga kuwe na onyesho la jinsi kitabu Biblia Inafundisha kinavyoweza kutolewa. Katika onyesho hilo zungumzia jambo linalowavutia watu katika eneo lenu.
Dak.15:Umuhimu wa Kufuata Wakati. Mazungumzo. (1) Yehova amewekaje mfano mzuri katika kufuata wakati? (Hab. 2:3) (2) Kufika mapema kwenye mikutano na utumishi wa shambani kunaonyeshaje kwamba tunamheshimu Yehova na tunawajali wengine? (3) Tunapochelewa kufika kwenye mkutano wa utumishi wa shambani, wale walio katika kikundi chetu cha utumishi wa shambani na yule anayeongoza mkutano huo, wanaathirikaje? (4) Tukimwahidi mtu anayependezwa au mwanafunzi wa Biblia kwamba tutarudi wakati fulani, kwa nini ni muhimu tufike wakati huo? (Mt. 5:37) (5) Ni mapendekezo gani yatakayotusaidia tutimize ahadi tunazotoa katika utumishi wa shambani na kufika kwa wakati kwenye mikutano ya kutaniko?
Wimbo 69 na Sala