“Nimekutembelea Ili . . .”
Wenye nyumba wanapofungua milango yao na kutuona, huenda wakashangaa na kujiuliza sisi ni nani na kwa nini tupo hapo. Tunaweza kusema nini katika utangulizi wetu ili kuwasaidia wasiwe na wasiwasi? Baada ya kuwasalimia, wahubiri fulani hutumia neno “ili” wakinuia kueleza kusudi la kuwatembelea. Kwa mfano, huenda wakasema hivi: “Tumekutembelea ili kuzungumzia jinsi uhalifu unavyowahangaisha watu wengi. Je, unafikiri . . .” au “Nimekutembelea ili kukuonyesha jinsi ya kujifunza Biblia bila malipo.” Ikiwa mwanzoni kabisa mwenye nyumba anaelezwa kwa nini tumemtembelea, huenda akawa tayari kusikiliza yale tunayotaka kusema.