Matangulizi ya Kuwafanya Wenye Nyumba Wasikilize
1 Ni nini iliyo sehemu ya maana zaidi katika utoaji wako wa nyumba kwa nyumba? Wengi wetu waweza kukubali kwamba ni utangulizi. Ikiwa hufanikiwi kuamsha kupendezwa kwa mwenye nyumba katika sekunde za kwanza 30 hivi, labda atakatiza mazungumzo.
2 Ni mambo gani upasayo kufikiria unapotayarisha utangulizi wenye matokeo? Changanua desturi na mahitaji ya watu uelekeao kuwapata. Je! ni desturi kusalimiana, au utatazamiwa ufikie jambo kuu upesi? Je! kuna wenzi wa ndoa wengi wachanga katika eneo lenu? Ni nini yaliyo mahangaiko yao? Je! watu katika ujirani wenu wanajua matatizo yanayokabili ainabinadamu kwa ujumla? Ikiwa ndivyo, huenda ukapenda kutumia Isaya 9:6, 7 na Mika 4:3, 4 na utoe kitabu Usalama Ulimwenguni Pote.
Huenda ukawafanya wasikilize kwa kusema jambo kama hili:
◼ “Habari ya asubuhi. Jina langu ni ______. Mimi huhangaishwa ninaposoma juu ya watu wanaoona njaa na wanaouawa katika vita. Na wewe je?” Maswali mengine ambayo yaweza kusaidia kuanzisha mazungumzo ni: “Ni nini lililo suluhisho kwa matatizo ya ulimwengu?” “Je! wafikiri mtu yeyote aweza kuridhisha tamaa yetu ya asili ya amani na usalama? Ona sifa zilizoorodheshwa hapa katika Isaya 9:6, 7 kwa utawala wa Ufalme wa Mungu. (Soma na ueleze andiko.)” “Wazia kama mtawala fulani angekuwa na sifa kama hizo zilizotajwa katika Isaya 9:6, 7? [Soma na ueleze andiko.]”
3 Katika maeneo fulani, huenda watu wakaonyesha hangaikio kubwa zaidi kwa nyumba na familia zao kuliko kwa mambo ya ulimwengu kama vile amani ya ulimwengu. Basi katika hali hiyo Kichwa cha Mazungumzo kilichoonyeshwa katika Huduma ya Ufalme Yetu ya Desemba 1991 chapasa kuwa chenye msaada. Zaidi ya utangulizi uliodokezwa katika makala hiyo,
Huenda ukaamsha kupendezwa kwa kuuliza:
◼ “Unaona maisha yatakuwaje kwako na kwa familia yako katika miaka kumi ijayo? Bila shaka unakubali kwamba mengi yatategemea maamuzi ya kibinafsi tunayofanya sasa. Biblia yaweza kufanya kazi katika kutusaidia kufanya maamuzi kama hayo kwani iliandikwa ili kutufundisha sisi hata katika karne ya 20. Ona yale Warumi 15:4 husema.”
4 Mfikio mwingine baada ya kujitambulisha waweza kuwa: “Swali ambalo tunauliza majirani zetu leo ni, “Ni wapi tunapoweza kupata msaada kikweli ili kuwezana na misongo ya maisha ya siku hizi? Je! kuna chochote ambacho chaweza kusaidia vijana wetu wafanye maamuzi ya hekima wanapokabiliwa na mambo mbalimbali? Je! kuna chanzo chenye kutegemeka cha mashauri mazuri juu ya kuendeleza mahusiano mazuri ya kibinafsi kazini, shuleni, au katika familia? Biblia ndiyo chanzo hicho kama tusomavyo hapa katika 2 Timotheo 3:16, 17.”
5 Sisi sote, kutia ndani na vijana wa umri wa kwenda shule, twaweza kutumia utoaji huo mbalimbali ulio sahili wa kutumia andiko moja. Kwa kweli, huenda ukapenda kujaribu mmoja unapotoa magazeti. Kumbuka kwamba, lengo letu ni kukadiria kupendezwa kwa mwenye nyumba kabla ya kumtolea fasihi. Je! hukubali kwamba toleo la Kimaandiko kama hilo lingekuwa njia bora ya kutambua kama msikilizaji wetu anadhihirisha upendezi wa kweli? Tuna hakika kwamba wengi wataonea shangwe kutumia utoaji huo mbalimbali katika Januari, wanapotoa magazeti na wanapotoa toleo la kawaida la mwezi pia.
6 Ukitumia sekunde za kwanza 30 kwa matokeo katika ziara yako, kwa mwenendo wako na utangulizi wako pia, utaelekea kutimiza lengo la maana la kuwafanya wenye nyumba wasikilize.