Je, Utaitumia Hii Fursa?
Ukumbusho Utatuwezesha Kuonyesha Shukrani
1.Ukumbusho hutokeza fursa gani ya pekee?
1 Ukumbusho utakaoadhimishwa Aprili 14 unatokeza fursa ya pekee ya kusitawisha na kuonyesha shukrani zetu kwa wema wa Yehova. Simulizi la Luka 17:11-18 hueleza jinsi Yehova na Yesu wanavyoona utoaji wa shukrani. Kwa kusikitisha, kati ya wale kumi wenye ukoma walioponywa ni mmoja tu aliyerudi kutoa shukrani. Wakati ujao, kupitia zawadi ya fidia, matatizo yote yatakomeshwa na hivyo tutaweza kuishi milele! Bila shaka, wakati huo tutamshukuru Yehova kila siku kwa baraka hizo. Hata hivyo tunawezaje kuonyesha shukrani zetu katika majuma yajayo?
2.Tunawezaje kuithamini fidia?
2 Sitawisha Uthamini: Mambo tunayofikiria hutuchochea kuonyesha shukrani. Ili kutusaidia tuithamini fidia, ratiba maalum inapatikana katika machapisho kadhaa, kama vile kalenda na kijitabu Kuyachunguza Maandiko Kila Siku. Kwa nini msizungumzie habari hiyo katika familia yenu? Kufanya hivyo kutatusaidia tuithamini fidia zaidi. Jambo hilo litatuchochea tuongeze bidii katika matendo mema.—2 Kor. 5:14, 15;1 Yoh.4:11.
3.Ni kwa njia gani tunaweza kuonyesha uthamini wetu katika majira ya Ukumbusho?
3 Onyesha Shukrani: Shukrani hudhihirishwa kwa matendo. (Kol. 3:15) Yule mwenye ukoma alijitahidi kumtafuta Yesu ili amshukuru. Bila shaka, aliwasimulia wengine kwa shauku jinsi alivyoponywa kimuujiza. (Luka 6:45) Je, tutaonyesha tunathamini fidia kwa kushiriki kwa bidii katika kampeni ya kuwaalika watu kwenye ukumbusho? Njia nyingine bora ya kuonyesha shukrani ni kufanya upainia msaidizi au kuongeza utumishi wetu katika majira ya Ukumbusho. Wakati wa Ukumbusho, uthamini wetu utatuchochea kuwakaribisha wageni na kuwa tayari kujibu maswali ambayo huenda wakauliza.
4.Tunawezaje kutumia fursa hii ya majira ya Ukumbusho bila kujuta?
4 Je, hii itakuwa mara ya mwisho kuadhimisha Ukumbusho? (1 Kor. 11:26) Hatujui. Lakini jambo tunalojua ni kwamba, ikiwa hiyo itakuwa mara ya mwisho, basi hatutakuwa na fursa nyingine tena ya kuonyesha shukrani zetu. Je, utatumia fursa hiyo? Tumfurahishe Yehova Mwandalizi wetu wa fidia kupitia maneno yetu ya shukrani na kwa kutafakari ukarimu wake kwa uandalizi huo.—Zab. 19:14.