Ratiba ya Juma Linaloanza Januari 19
JUMA LINALOANZA JANUARI 19
Wimbo 47 na Sala
Funzo la Biblia la Kutaniko:
cl sura ya 19 ¶1-8 (Dak. 30)
Shule ya Huduma ya Kitheokrasi:
Usomaji wa Biblia: Waamuzi 1-4 (Dak. 8)
Na. 1: Waamuzi 3:1-11 (Isizidi dak. 3)
Na. 2: Unawezaje Kujifunza Kumhusu Mungu?—igw uku. 4 ¶1-4 (Dak. 5)
Na. 3: Wakristo wa Kweli Hawaoi Wake Wengi—td 26E (Dak. 5)
Mkutano wa Utumishi:
Kichwa cha Mwezi Huu: ‘Mtumikie Bwana kwa unyenyekevu mkubwa.’—Mdo. 20:19.
Dak. 10: Je, Unatumia Mwongozo wa Kujifunza Neno la Mungu? Mazungumzo yanayotegemea maswali yafuatayo: (1) Kijitabu Mwongozo wa Kujifunza Neno la Mungu kinawezaje kutusaidia tunaposoma (a) Waamuzi 16:1-3 (b) Luka 6:17, na (c) Waroma 15:19? (2) Kijitabu hicho kinawezaje kutusaidia kuelewa vizuri maneno kama vile (a) “omeri” na “efa (Kut. 16:32, 36),” (b) “talanta (Mt. 25:15),” na (c) “Abibu” na “Nisani (Kum. 16:1)”? Malizia kwa kuwatia moyo wote watumie kifaa hicho. Ikiwa kijitabu Mwongozo wa Kujifunza Neno la Mungu hakipatikani, onyesha jinsi wahubiri wanavyoweza kunufaika kwa kutumia nyongeza iliyo katika Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Kiswahili, ukitumia habari zinazozungumzia “Jina la Mungu,” “Gehena,” na “Nafsi.”
Dak. 10: Kumtumikia Bwana Kunahitaji Utayari na Uvumilivu. Mazungumzo yanayotegemea Kitabu cha Mwaka—2014, ukurasa wa 59, fungu la 1, hadi ukurasa wa 62, fungu la 1; na ukurasa wa 67, fungu la 2. Waombe wasikilizaji waeleze mambo waliyojifunza.
Dak. 10: “Endelea Kufanya Maendeleo Ukiwa Mhudumu.” Maswali na majibu.
Wimbo 20 na Sala