Kutangaza kwa Bidii Ukweli Kumhusu Yesu
Tunapojua jinsi ya kuwahubiria wengine kumhusu Yesu, bidii yetu huongezeka zaidi. Yesu ni jiwe la msingi la pembeni na imani ya kweli inajengwa juu yake. (Efe. 2:20) Bila yeye, tusingekuwa na tumaini la uzima. (Mdo. 4:12) Kwa hiyo, ni muhimu sote tutambue sehemu ambayo Yesu anatimiza katika kusudi la Mungu. Wengi wamepotoshwa na mafundisho yasiyo ya kimaandiko. Kwa kusikitisha, huenda wasifaidike na ahadi ambazo Mungu amewaahidi wale wanaomwamini Yesu. Bidii yetu itatuchochea tuwasaidie watu wenye mioyo minyoofu kupata ujuzi sahihi kumhusu Yesu, waelewe uhusiano wake pamoja na Mungu, na sehemu yake katika kusudi la Mungu. Je, utatangaza kwa bidii ukweli kumhusu Yesu katika majira haya ya Ukumbusho?