Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi
Mnara wa Mlinzi Agosti 1
“Tunawatembelea jirani zetu kwa ufupi tukiwa na ujumbe utakaowasaidia kushughulika na matatizo yanayowahangaisha watu wengi. Tatizo moja gumu kushughulika nalo ni kifo cha mpendwa wetu. Je, unakubali jambo hilo? [Mruhusu ajibu.] Ona ahadi hii ya Biblia yenye kutia moyo. [Soma Ufunuo 21:3, 4.] Biblia inatoa tumaini kwamba siku moja wapendwa wetu waliokufa wataishi tena. Gazeti hili linaeleza jinsi jambo hilo litakavyotimizwa.”
Amkeni Agosti
“Tunawaonyesha jirani zetu makala ambayo inazungumzia habari nyingi sana zilizo kwenye chembe za mwili wetu. [Mwonyeshe ukurasa wa juu wa gazeti la Amkeni!] Wengi hufikiri kwamba uhai ulijitokeza kupitia mageuzi, ilhali wengine wanafikiri kwamba kuna Muumba. Wewe una maoni gani? [Mruhusu ajibu.] Gazeti hili linaeleza uvumbuzi wenye kustaajabisha kuhusu chembe hizo, ambao umewafanya baadhi ya wanasayansi watilie shaka fundisho la mageuzi.”