Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi
Mnara wa Mlinzi Januari 1
“Inaonekana kwamba sikuzote kumekuwa na tatizo la ufisadi katika serikali. Unafikiri ni kwa nini hali iko hivyo? [Mruhusu ajibu.] Ningependa kukuonyesha jambo fulani lenye kupendeza linalopatikana katika Biblia. [Soma Mhubiri 7:20.] Gazeti hili linazungumzia suluhisho la ufisadi kutoka katika Biblia. Tafadhali tenga wakati fulani wa kusoma gazeti hili. Hii ni nakala yako.”
Amkeni Januari
“Watu wengi wanaamini kwamba uhai ulitokana na mageuzi, ilihali wengine hawana uhakika. Unafikiri uhai ulianzaje? [Mruhusu ajibu.] Utafiti uliofanywa kwa miaka mingi unaonyesha kuwa uhai unaweza kutokezwa tu na uhai mwingine. Jambo hilo linapatana na mstari huu wa Biblia. [Soma Zaburi 36:9.] Gazeti hili linaeleza kwa nini watu wengi wamefikia mkataa kuwa ni vigumu sana kwa mageuzi kutokeza uhai, ambao ni tata na wenye kustaajabisha.”