Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi
Mnara wa Mlizi Juni 1
“Tunawatembelea jirani zetu kwa muda mfupi ili kuwachochea wapendezwe na Biblia. Watu wengi wanafikiri kwamba sayansi ya kisasa inathibitisha kwamba Biblia si sahihi. Wewe una maoni gani kuhusu Biblia? Je, unafikiri inaweza kutumainika? [Mruhusu ajibu.] Ona mfano huu mzuri unaoonyesha jinsi Biblia ilivyo sahihi kisayansi. [Soma Ayubu 26:7.] Gazeti hili linazungumzia upatano uliopo kati ya sayansi na Biblia.”
Amkeni Juni
“Kwa sababu watu wengi wanakabili matatizo ya kiafya, tunawatembelea kwa muda mfupi ili kuzungumzia andiko hili linalotia moyo. [Soma Isaya 33:24a.] Unafikiri maisha yetu yangekuwaje ikiwa hakungekuwa na magonjwa? [Mruhusu ajibu.] Tunaposubiri utimizo wa ahadi hiyo, kuna mambo matano muhimu tunayoweza kufanya ili kuboresha afya zetu. Gazeti hili linaeleza mambo hayo.”