Ratiba ya Juma Linaloanza Septemba 21
JUMA LINALOANZA SEPTEMBA 21
Wimbo 53 na Sala
Funzo la Biblia la Kutaniko:
cl sura ya 30 ¶19-23, sanduku kwenye uku. 309 (Dak. 30)
Shule ya Huduma ya Kitheokrasi:
Usomaji wa Biblia: 2 Wafalme 19-22 (Dak. 8)
Na. 1: 2 Wafalme 20:12-21 (Isizidi dak. 3)
Na. 2: Tunda Lililokatazwa Lilikuwa Nini?—td 3C (Dak. 5)
Na. 3: Neno “Amina” Linamaanisha Nini? (Dak. 5)
Mkutano wa Utumishi:
Kichwa cha Mwezi Huu: ‘Toa ushahidi kamili kuhusu habari njema.’ —Mdo. 20:24.
Dak. 10: Tulitimiza Nini Katika Mwaka wa Utumishi Uliopita? Hotuba. Itolewe na mwangalizi wa utumishi. Zungumzia utendaji wa kutaniko wa mwaka wa utumishi uliopita. Kazia mambo mazuri yaliyotimizwa na uwapongeze wahubiri. Taja sehemu moja au mbili za huduma ambazo kutaniko linaweza kufanyia kazi katika mwaka huu wa utumishi, na utoe mapendekezo yanayofaa.
Dak. 10: Kutoa Ushahidi Kamili Huwa na Matokeo Mazuri. Mazungumzo yanayotegemea Kitabu cha Mwaka 2015, ukurasa wa 54, fungu la 1; ukurasa wa 56, fungu la 2, hadi ukurasa wa 57, fungu la 1; na ukurasa wa 63, fungu la 2, hadi ukurasa wa 64, fungu la 1. Baada ya kuzungumzia mambo hayo yaliyoonwa, waombe wasikilizaji waeleze mambo waliyojifunza. Mahali ambapo Kitabu cha Mwaka hakipatikani katika lugha inayotumiwa na kutaniko, sehemu hii ishughulikiwe na mzee au mtumishi wa huduma ambaye ana Kitabu cha Mwaka katika lugha nyingine. Ikiwa baadhi ya wahubiri wana kitabu hicho katika lugha tofauti, wanaweza kutiwa moyo wakitumie na wawasaidie wengine waelewe mambo tunayojifunza.
Dak. 10: “Igeni Imani Yao.” Maswali na majibu. Mahali ambapo machapisho tofauti yatatumiwa, watie moyo wajitayarishe mapema na kushiriki. Kazia mambo makuu machache yaliyo katika kitabu hicho.
Wimbo 81 na Sala