HAZINA ZA NENO LA MUNGU | ZABURI 11-18
Ni Nani Atakayekuwa Mgeni Katika Hema la Yehova?
Kuwa mgeni katika hema la Yehova kunamaanisha kwamba mtu ni rafiki ya Mungu, anamtegemea, na kumtii. Zaburi 15 inaeleza aina ya rafiki ambaye Yehova anakubali.
MGENI WA YEHOVA LAZIMA . . .
awe mtimilifu
aseme kweli, hata katika moyo wake
awaheshimu watumishi wenzake wa Yehova
atimize ahadi, hata chini ya hali ngumu
awasaidie wenye uhitaji bila kutarajia malipo
MGENI WA YEHOVA ANAEPUKA . . .
porojo na uchongezi
kumfanyia mwenzake jambo lolote baya
kuwatumia vibaya ndugu zake Wakristo
kushirikana na wale ambao hawamtumikii wala kumtii Yehova
kuchukua rushwa