Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mwbr16 Novemba kur. 1-2
  • Marejeo ya Daftari la Huduma na Maisha

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Marejeo ya Daftari la Huduma na Maisha
  • Marejeo ya Daftari la Huduma na Maisha—2016
  • Vichwa vidogo
  • NOVEMBA 7-13
Marejeo ya Daftari la Huduma na Maisha—2016
mwbr16 Novemba kur. 1-2

Marejeo ya Daftari la Huduma na Maisha

NOVEMBA 7-13

HAZINA ZA NENO LA MUNGU | METHALI 27-31

it-2 1183

Mke

Sheria yamlinda mke. Ingawa mume alikuwa na mamlaka ya juu zaidi katika mpango wa ndoa, maagizo ya Mungu yalikuwa kwamba mume alipaswa kuitunza na kuiandalia familia yake mahitaji ya kimwili na kiroho. Pia, aliwajibika kutokana na makosa yoyote yaliyofanywa na familia; hivyo alikuwa na daraka zito. Na ingawa alikuwa na mapendeleo mengi zaidi kuliko mke wake, sheria ya Mungu ilimlinda mke na kumpa mapendeleo fulani ya pekee, jambo hilo lilimwezesha mke kuwa na maisha yenye furaha na ufanisi.

Ifuatayo ni mifano michache ya ulinzi ambao mke alipata kupitia sheria: Hukumu ya kifo kwa sababu ya kufanya uzinzi ilitolewa kwa yeyote aliyekuwa na hatia iwe ni mke au mume. Ikiwa mume alitilia shaka uaminifu wa mke wake, angeweza kumleta kwa kuhani, ili Yehova ahukumu jambo hilo, na ikiwa angeonekana kuwa na hatia, viungo vyake vya uzazi vingeharibika; kwa upande mwingine, ikiwa angekuwa hana hatia, mume wake alipaswa kumpa mimba, na hivyo kuonyesha kwa watu wote kwamba hana hatia. (Hes 5:​12-31) Mume angeweza kumpa cheti cha talaka mke wake ikiwa amepata kitu fulani kisichofaa katika mwanamke huyo. Huenda hilo lilitia ndani mke kumvunjia heshima mume wake au kuiletea suto nyumba yake au ya baba mkwe wake. Lakini Sheria ilimlinda mke huyo kwa kutoa agizo kwamba mume anapaswa kumwandikia mke huyo cheti cha talaka. Kisha angekuwa huru kuolewa na mwanamume mwingine. (Kum 24:​1, 2) Ikiwa mke aliweka nadhiri ambayo mume wake aliiona kuwa haifai au ingeathiri hali njema ya familia, angeweza kuifuta. (Hes 30:10-15) Uandalizi huo uliwekwa ili kumsaidia mke, kumlinda dhidi ya maamuzi yake yoyote ambayo yangemwingiza kwenye matatizo.

Ndoa za wake wengi ziliruhusiwa chini ya Sheria ya Musa lakini miongozo ilihakikisha kwamba haki za mke zinalindwa. Mume hangeweza kuhamisha haki ya mzaliwa wa kwanza kwenda kwa mwana wa kwanza wa mke aliyependwa zaidi. (Kum 21:15-17) Ikiwa binti Mwisraeli angeuzwa na baba yake awe kijakazi na bwana wake amfanye kuwa suria wake, kisha bwana huyo aache kupendezwa naye, basi angeruhusu binti huyo akombolewe, lakini hakuruhusiwa kumuuza kwa watu wa kigeni. (Kut 21:7, 8) Ikiwa bwana huyo au mwana wake alimfanya binti huyo kuwa suria na kisha kuchukua mke mwingine, binti huyo alipaswa kuandaliwa chakula, mavazi, malazi, na kupewa haki yake ya ndoa.​—Kut 21:9-11.

Ikiwa kwa hila mume alimshtaki mke wake kwa kudai kwamba wakati wa kufunga ndoa alisema uwongo kuwa yeye ni bikira na ithibitishwe kwamba shtaka hilo si la kweli, mume huyo angeadhibiwa na alipaswa kumlipa baba ya msichana huyo thamani ya pesa iliyo mara mbili ya bei ya kununua bikira na hakuruhusiwa kamwe kumtaliki siku zake zote. (Kum 22:13-19) Ikiwa mwanamume angemshawishi msichana bikira ambaye hajachumbiwa, alipaswa kulipa bei ya kununua bikira kwa baba ya msichana huyo na, ikiwa baba huyo angemruhusu, angemwoa, lakini hangeruhusiwa kamwe kumtaliki siku zake zote.​—Kum 22:28, 29; Kut 22:16, 17.

Ingawa mke katika jamii ya Waebrania alikuwa na hali zinazotofautiana kwa njia fulani na hali za mke katika nchi za Magharibi leo, mke mwaminifu wa Kiebrania alifurahia daraka hilo na kazi yake. Alimsaidia mume wake, alilea familia, alitunza nyumba yake, na alikuwa na mengi yaliyomletea uradhi na furaha, akiwa na fursa kamili ya kutumia vipaji vyake akiwa mwanamke.

Ufafanuzi wa Mke Mwema. Furaha na utendaji mbalimbali wa mke mwaminifu umefafanuliwa katika Methali 31. Mke huyo anasemwa kuwa ni mwenye thamani inayopita ile ya marijani machoni pa mume wake. Mume wake anaweza kumtegemea. Mke huyo anafanya kazi kwa bidii​—anafuma, anatengeneza nguo kwa ajili ya familia yake, anafanya ununuzi kwa ajili ya nyumba yake, anafanya kazi katika shamba la mizabibu, anasimamia wafanyakazi wa nyumbani, anatoa msaada kwa wenye uhitaji, anaivisha familia yake nguo zenye kupendeza, hata anasaidia kupata pesa kwa ufumaji wake, anaitayarisha familia yake kwa dharura za wakati ujao, anajieleza kwa njia ya hekima na kwa fadhili zenye upendo, na, kwa sababu ya kumwogopa Yehova na kufanya kazi kwa bidii, amejipatia sifa kutoka kwa mume wake na wana wake, na hivyo anamletea heshima mume wake na familia yake katika nchi. Kwa hakika, mtu aliyepata mke mwema amepata kitu chema na hupata nia njema kutoka kwa Yehova.​—Met 18:22.

Katika Kutaniko la Kikristo. Mwongozo kwa Kutaniko la Kikristo ni kwamba mume anapaswa kuwa na mke mmoja tu. (1Ko 7:2; 1Ti 3:2) Wake wanaagizwa wajitiishe kwa waume zao, iwe waume hao ni watumishi wa Yehova au la. (Efe 5:22-24) Wake hawapaswi kuwanyima waume zao haki yao ya ndoa, kwa kuwa kama ilivyo kwa mume, ndivyo ilivyo kwa mke, hana “mamlaka juu ya mwili wake mwenyewe.” (1Ko 7:3, 4) Wake wanaagizwa kwamba kujipamba kwao kuwe kwa yule mtu wa siri wa moyoni, wakidhihirisha tunda la roho, ili waume wao wasioamini wavutwe kupitia mwenendo wao na kuwa Wakristo.​—1Pe 3:1-6.

Njia ya Mfano. Katika njia ya mfano, Yehova aliliona taifa la Israeli kuwa mke wake kwa sababu ya agano ambalo alifanya na taifa hilo. (Isa 54:6) Mtume Paulo humrejelea Yehova kuwa Baba ya Wakristo waliozaliwa kwa roho, na anazungumzia “Yerusalemu la juu” kuwa ni mama yao, kana kwamba Yehova ni mume wake kwa kusudi la kutokeza Wakristo waliozaliwa kwa roho. (Gal 4:​6, 7, 26) Kutaniko la Kikristo linazungumziwa kana kwamba ni bibi-arusi, au mke, wa Yesu Kristo.​—Efe 5:​23, 25; Ufu 19:7; 21:​2, 9.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki