MAISHA YA MKRISTO
Watayarishe Watoto Wako Wamfuate Kristo
Hakuna kitu kinachowapa shangwe wazazi Wakristo kama kumwona mtoto wao ‘akijikana mwenyewe, akiubeba mti wake wa mateso na kuendelea kumfuata’ Yesu. (Mk 8:34; 3Yo 4) Wazazi wanaweza kufanya nini ili kuwatayarisha watoto wao wamfuate Yesu, wajiweke wakfu kwa Yehova, na kubatizwa? Ni mambo gani ambayo huenda yakaonyesha kwamba mtoto wako yuko tayari kuchukua hatua muhimu ya ubatizo?
Someni “Ujumbe kwa Wazazi Wakristo” kwenye ukurasa wa 165-166 wa kitabu Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova, kisha mzungumzie maswali yafuatayo: