MAISHA YA MKRISTO
Fuata Hatua za Kristo kwa Ukaribu
Yesu alituwekea mfano wa kuiga, hasa tunapokabili majaribu au mateso. (1Pe 2:21-23) Ingawa Yesu alitukanwa, hakulipiza, hata alipokuwa akiteswa. (Mk 15:29-32) Ni nini kilichomsaidia kuvumilia? Aliazimia kufanya mapenzi ya Yehova. (Yoh 6:38) Pia, alikazia fikira “shangwe iliyowekwa mbele yake.”—Ebr 12:2.
Tunatendaje tunapoteswa kwa sababu ya imani yetu? Wakristo wa kweli ‘hawalipi uovu kwa uovu.’ (Ro 12:14, 17) Tunapomwiga Yesu kwa kuvumilia mateso, tunaweza kushangilia kwamba tuna kibali cha Mungu.—Mt 5:10-12; 1Pe 4:12-14.
TAZAMENI VIDEO JINA LA YEHOVA NDILO MUHIMU ZAIDI, KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:
Dada Pötzingera alitumiaje wakati wake kwa hekima alipokuwa katika kifungo cha upweke?
Ndugu na Dada Pötzinger walivumilia mateso gani walipokuwa katika kambi mbalimbali za mateso?
Ni nini kilichowasaidia kuvumilia?
Unapoteswa, fuata hatua za Kristo kwa ukaribu
a Jina lake pia linaandikwa Poetzinger.