MAISHA YA MKRISTO
Shangilia Unapoteswa
Wakristo wanatarajia kwamba wanaweza kuteswa. (Yoh 15:20) Ingawa mateso yanaweza kutuletea mahangaiko na nyakati nyingine maumivu, tunaweza kupata shangwe tunapovumilia.—Mt 5:10-12; 1Pe 2:19, 20.
TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA TUNAWEZA KUWA NA SHANGWE LICHA YA MATESO, KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:
Ulijifunza nini kutokana na simulizi la Ndugu Bazhenov kuhusu umuhimu wa
kusoma Biblia kila siku?
kupokea msaada kutoka kwa Wakristo wenzako?a
kusali mara nyingi?
kuimba nyimbo za Ufalme?
kuwaeleza wengine kuhusu imani yetu?
a Tunaweza kusali kwa ajili ya Wakristo waliofungwa, hata tunaweza kutaja majina yao. Hata hivyo, ofisi ya tawi haiwezi kuwapelekea barua za kibinafsi tulizowaandikia.