MAISHA YA MKRISTO
Unaweza Kufaulu Licha ya Kuwa na “Mwiba Katika Mwili”!
Katika siku hizi za mwisho zenye hatari, matatizo yaliyo kama miiba yanawapata watumishi wote wa Mungu. (2Ti 3:1) Tunaweza kufanya nini ili kumtegemea Yehova na kukabiliana na matatizo yetu kwa mafanikio? Tazama video “Macho ya Vipofu Yatafunguliwa” ili kujua kile ambacho Talita Alnashi na wazazi wake wamefanya, kisha mjibu maswali yafuatayo:
Talita ana ‘mwiba gani katika mwili’?
Ni ahadi zipi za Biblia zilizomsaidia Talita na wazazi wake kuwa na mtazamo unaofaa?
Wazazi wa Talita walionyeshaje kwamba walimtegemea Yehova muda mfupi baada ya upasuaji wake?
Wazazi wa Talita wametumiaje vizuri vifaa vya kitheokrasi ili kumchochea Talita ampende Mungu kutoka moyoni?
Talita ameonyeshaje kwamba anakua kiroho licha ya kuwa na “mwiba katika mwili”?
Mfano wa Talita umekutiaje moyo?