Marejeo ya Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha
MEI 6-12
HAZINA ZA NENO LA MUNGU | 2 WAKORINTHO 4-6
“Hatufi Moyo”
it-1 724-725
Uvumilivu
Ni muhimu sana pia kwamba tusisahau kamwe tumaini letu la Kikristo, uzima wa milele bila dhambi. Hata tukiuawa na watu wanaotutesa hawawezi kutuondolea tumaini hilo. (Ro 5:4, 5; 1Th 1:3; Ufu 2:10) Mateso ya sasa si kitu kabisa yanapolinganishwa na kutimizwa kwa tumaini hilo la pekee. (Ro 8:18-25) Ingawa huenda mateso yakaonekana kuwa makali, yanapolinganishwa na umilele ni ‘ya muda mfupi na mepesi.’ (2Ko 4:6-18) Mtu anapokumbuka kwamba majaribu ni ya muda mfupi na ashikamane na tumaini lake la Kikristo, hatakata tamaa na kukosa kuwa mwaminifu kwa Yehova Mungu.
MEI 20-26
HAZINA ZA NENO LA MUNGU | 2 WAKORINTHO 11-13
Kutafuta Hazina za Kiroho
it-2 177
Busu
“Busu Takatifu.” Miongoni mwa Wakristo wa mapema kulikuwa na “busu takatifu” (Ro 16:16; 1Ko 16:20; 2Ko 13:12; 1Th 5:26) au “busu la upendo” (1Pe 5:14), ambalo huenda lilitolewa kati ya watu wa jinsia moja. Huenda aina hiyo ya salamu ya Wakristo wa mapema ikafanana na zoea la kale la Waebrania la kusalimiana kwa busu. Ingawa Maandiko hayafunui habari hususa kulihusu, ni wazi kwamba “busu takatifu” au “busu la upendo” lilionyesha upendo na umoja uliokuwepo katika kutaniko la Kikristo.—Yoh 13:34, 35.
MEI 27–JUNI 2
HAZINA ZA NENO LA MUNGU | WAGALATIA 1-3
“Nilimpinga Uso kwa Uso”
it-2 587 fu. 4
Paulo
Muda fulani baada ya hapo, Petro mwenyewe alikuja Antiokia ya Siria na akashirikiana na Wakristo Wasio Wayahudi. Lakini, Wayahudi fulani walipofika kutoka Yerusalemu, aliacha kushirikiana na wasio Wayahudi, kwa kuwa alijiruhusu kuwaogopa wanadamu na hivyo akatenda tofauti na mwongozo wa roho ulioonyesha kwamba tofauti za kimwili hazina maana yoyote mbele za Mungu. Hata Barnaba aliongozwa vibaya. Paulo alipotambua hilo, alimkemea Petro mbele ya watu, kwa kuwa mwenendo wake ulikuwa ukienda kinyume na maendeleo ya Ukristo.—Gal 2:11-14.
Kutafuta Hazina za Kiroho
it-1 880
Wagalatia, Barua kwa
Paulo aliposema kwa mshangao, “Enyi Wagalatia wasio na akili,” hakuna uthibitisho kwamba alikuwa akiwafikiria watu wa kabila fulani pekee ambao walitoka hasa upande wa kaskazini wa Galatia. (Gal 3:1) Badala ya hivyo, Paulo alikuwa akiwakemea baadhi ya watu kutanikoni kwa kujiruhusu waathiriwe na watu wa dini ya Kiyahudi waliokuwa miongoni mwao ambao walijaribu kuthibitisha uadilifu wao kupitia Sheria ya Musa badala ya ‘kutangazwa kuwa waadilifu kupitia imani’ iliyoandaliwa na agano jipya. (Gal 2:15–3:14; 4:9, 10) “Makutaniko ya Galatia” (1:2) ambayo Paulo aliyaandikia yalikuwa na mchanganyiko wa Wayahudi na wasio Wayahudi. Watu hao wasio Wayahudi walitia ndani wageuzwa-imani waliotahiriwa na Watu wa Mataifa wasiotahiriwa, na bila shaka baadhi yao walikuwa Waselti. (Mdo 13:14, 43; 16:1; Gal 5:2) Kwa ujumla, waliitwa Wakristo Wagalatia kwa sababu eneo ambalo waliishi liliitwa Galatia. Kusudi kuu la barua ya Paulo ni kuwaandikia wale aliowafahamu vizuri katika eneo la kusini la jimbo hilo la Roma, na si kwa watu ambao hakuwajua kabisa katika eneo la kaskazini ambako inaonekana hakuwahi kutembelea.