Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mwbr19 Juni kur. 1-2
  • Marejeo ya Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Marejeo ya Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha
  • Marejeo ya Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha—2019
  • Vichwa vidogo
  • JUNI 3-​9
  • JUNI 10-16
  • JUNI 17-23
  • JUNI 24-30
Marejeo ya Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha—2019
mwbr19 Juni kur. 1-2

Marejeo ya Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha

JUNI 3-​9

HAZINA ZA NENO LA MUNGU | WAGALATIA 4-6

“‘Tukio la Mfano’ Linalotuelimisha”

it-1 1018 ¶2

Hagari

Kulingana na mtume Paulo, Hagari alishiriki tukio la mfano akiwakilisha taifa la Israeli la asili lililounganishwa na Yehova kupitia agano la Sheria lililoanzishwa rasmi katika Mlima Sinai, na agano hilo lilitokeza “watoto kwa ajili ya utumwa.” Kwa sababu ya hali ya dhambi ya watu, taifa hilo lilishindwa kufuata matakwa ya agano hilo. Chini ya agano hilo, Waisraeli hawakuwa huru bali walihukumiwa kuwa watenda-dhambi waliostahili kifo; hivyo, walikuwa watumwa. (Yoh 8:34; Ro 8:1-3) Yerusalemu la siku za Paulo liliwakilisha Hagari, kwa kuwa mji mkuu Yerusalemu, uliowakilisha Israeli la asili, ulijikuta utumwani pamoja na watoto wake. Hata hivyo, Wakristo waliotiwa mafuta kwa roho ni watoto wa “Yerusalemu la juu,” mwanamke wa mfano wa Mungu. Kama Sara mwanamke aliye huru, Yerusalemu hilo halijawahi kuwa mtumwa. Lakini kama Isaka alivyonyanyaswa na Ishmaeli, vivyo hivyo watoto wa “Yerusalemu la juu,” ambao wamewekwa huru na Mwana, wamenyanyaswa mikononi mwa watoto wa Yerusalemu lililo utumwani. Hata hivyo, Hagari na mwana wake walifukuzwa, jambo linalowakilisha jinsi Yehova alivyolikataa Israeli la asili likiwa taifa.—Gal 4:21-31; ona pia Yoh 8:31-40.

JUNI 10-16

HAZINA ZA NENO LA MUNGU | WAEFESO 1-3

“Mpango wa Usimamizi wa Yehova na Kazi Yake”

it-2 837 ¶4

Siri Takatifu

Ufalme wa Kimasihi. Katika maandishi ya Paulo anaeleza kikamili kuhusu kufunuliwa kwa siri takatifu kuhusu Kristo. Katika Waefeso 1:9-11, anazungumzia jinsi Mungu alivyofunua “siri takatifu” ya mapenzi yake, na kusema: “Ni kulingana na mapenzi yake mema aliyokusudia mwenyewe kwa ajili ya usimamizi kwenye nyakati kamili zilizowekwa, kukusanya pamoja vitu vyote katika Kristo, vitu vilivyo mbinguni na vitu vilivyo duniani. Ndiyo, katika yeye ambaye tuko katika muungano naye na tulihesabiwa kuwa warithi, kwa kuwa tuliagizwa awali kulingana na kusudi la yule anayetimiza mambo yote kama anavyoamua kulingana na mapenzi yake.” Hiyo “siri takatifu” inahusisha serikali, yaani, Ufalme wa Kimasihi wa Mungu. “Vitu vilivyo mbinguni,” ambavyo Paulo anarejelea, ni warithi watarajiwa wa Ufalme wa mbinguni wakiwa pamoja na Kristo. “Vitu vilivyo duniani” ni raia wa kidunia wa Ufalme huo. Yesu aliwaeleza wanafunzi wake kwamba siri takatifu inahusiana na Ufalme alipowaambia hivi: “Ninyi mmepewa siri takatifu ya Ufalme wa Mungu.”—Mk 4:11.

JUNI 17-23

Kutafuta Hazina za Kiroho

it-1 1128 ¶3

Utakatifu

Roho takatifu. Nguvu ya utendaji ya Yehova au roho yake, inadhibitiwa naye na inatimiza kusudi lake sikuzote. Ni safi, takatifu, na imetengwa kwa matumizi mema ya Mungu. Hivyo, inaitwa “roho takatifu” na “roho ya utakatifu.” (Zb 51:11; Lu 11:13; Ro 1:4; Efe 1:13) Roho takatifu inapotenda ndani ya mtu inakuwa nguvu ya utakatifu au usafi. Zoea lolote lisilo safi au lisilofaa linapinga au ‘kuihuzunisha’ roho hiyo. (Efe 4:30) Ingawa si mtu, roho takatifu ni wonyesho wa utu mtakatifu wa Mungu na hivyo inaweza ‘kuhuzunishwa.’ Kuzoea kufanya dhambi ya aina yoyote “[kunauzima] moto wa roho.” (1Th 5:19) Zoea kama hilo likiendelea, roho takatifu ya Mungu inaweza “kutiwa uchungu,” na hilo linaweza kufanya Mungu ageuke na kuwa adui ya mtu huyo aliyeasi. (Isa 63:10) Mtu anayeihuzunisha roho takatifu anaweza kufikia hatua ya kuikufuru, dhambi ambayo Yesu Kristo alisema haitasamehewa katika mfumo wa mambo wa sasa wala ule utakaokuja.—Mt 12:31, 32; Mk 3:28-30; ona ROHO.

it-1 1006 ¶2

Pupa

Inaonekana Kupitia Matendo. Pupa huonekana kupitia tendo fulani la wazi linalofunua tamaa ya mtu isiyofaa na iliyopita kiasi. Mwandikaji wa Biblia Yakobo anatueleza kwamba tamaa mbaya wakati imetunga mimba, huzaa dhambi. (Yak 1:14, 15) Hivyo, mtu mwenye pupa anaweza kujulikana kupitia matendo yake. Mtume Paulo anasema kwamba kuwa mwenye pupa kunamaanisha kuabudu sanamu. (Efe 5:5) Kwa sababu ya pupa mtu kama huyo anafanya kitu anachotamani kiwe mungu wake, na kukitanguliza badala ya utumishi na ibada kwa Muumba.—Ro 1:24, 25.

JUNI 24-30

Kutafuta Hazina za Kiroho

it-2 528 ¶5

Matoleo

Matoleo ya kinywaji. Mara nyingi matoleo ya kinywaji yalitolewa pamoja na matoleo mengine, hasa baada ya Waisraeli kukaa katika Nchi ya Ahadi. (Hes 15:2, 5, 8-10) Matoleo hayo yalitia ndani divai (“kileo”) na yalimiminwa juu ya madhabahu. (Hes 28:7, 14; linganisha Kut 30:9; Hes 15:10.) Mtume Paulo aliwaandikia hivi Wakristo jijini Filipi: “Ikiwa ninamiminwa kama toleo la kinywaji juu ya dhabihu na utumishi mtakatifu ambao imani yenu imewaongoza, ninafurahi.” Hapo alitumia mfano wa toleo la kinywaji kuonyesha utayari wake wa kujitoa kabisa kwa ajili ya Wakristo wenzake. (Flp 2:17) Muda mfupi kabla ya kifo chake, alimwandikia Timotheo hivi: “Mimi tayari ninamiminwa kama toleo la kinywaji, na wakati wangu wa kufunguliwa umekaribia sana.”—2Ti 4:6.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki