HAZINA ZA NENO LA MUNGU | MWANZO 9-11
“Dunia Yote Iliendelea Kuwa na Lugha Moja”
Huko Babeli, Yehova aliwatawanya wanadamu waasi kwa kuvuruga lugha yao. Leo anakusanya umati mkubwa kutoka kwa mataifa na lugha zote na kuwapa “lugha safi” ili “waweze kuliitia jina la Yehova, [na] wamtumikie bega kwa bega.” (Sef 3:9; Ufu 7:9) “Lugha safi” ni ukweli kumhusu Yehova na kusudi lake kama linavyoonyeshwa kwenye Maandiko.
Kujifunza lugha mpya kunahusisha mambo mengi zaidi ya kukariri tu maneno mapya. Kunahusisha kujifunza njia mpya ya kufikiri. Vivyo hivyo, tunapojifunza lugha mpya ya kweli, akili zetu zinageuzwa. (Ro 12:2) Hilo ni jambo la kuendelea ambalo hutokeza umoja kati ya watu wa Mungu.—1Kor 1:10.