MAISHA YA MKRISTO
Msifu Yehova Ukiwa Painia
Waisraeli walikuwa na sababu nzuri za kumsifu Yehova. Aliwakomboa kutoka Misri na kuwakomboa kutokana na jeshi la Farao! (Kut 15:1, 2) Yehova anaendelea kuwatendea watu wake mema. Tunaweza kuonyeshaje kwamba tunashukuru?—Zb 116:12.
Njia moja ni ya kufanya upainia msaidizi au wa kawaida. Unaweza kusali ili upate hamu na nguvu za kutumikia ukiwa painia. (Flp 2:13) Wengi huanza kwa kufanya upainia msaidizi. Machi na Aprili na katika mwezi ambao kuna ziara ya mwangalizi unaweza kuchagua kutimiza takwa la saa 30 au 50. Unapojionea shangwe ya kutumikia ukiwa painia msaidizi huenda ukatamani kutumikia ukiwa painia wa kawaida. Hata wale wanaofanya kazi wakati wote au wenye matatizo ya afya wamefaulu kuwa mapainia wa kawaida. (mwb16.07 8) Bila shaka, tunapaswa kufanya yote tunayoweza ili kumsifu Yehova.—1Nya 16:25.
TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA DADA WATATU NCHINI MONGOLIA, KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:
Dada hao watatu walikabiliana na changamoto zipi ili wawe mapainia?
Wamepata baraka zipi?
Baada ya wao kuwa mapainia wa kawaida, ni fursa zipi za kuongeza utumishi zilizojitokeza?
Mfano wao mzuri umewachocheaje wengine?