MAISHA YA MKRISTO
“Msihangaike”
Yehova aliwasaidia maskini katika Israeli la kale. Yeye huwasaidiaje watumishi wake ambao ni maskini leo?
Amewafundisha kuwa na maoni yenye usawaziko kuhusu pesa.—Lu 12:15; 1Ti 6:6-8.
Amewafundisha kujiheshimu.—Ayu 34:19.
Amewafundisha kufanya kazi kwa bidii na kuepuka mazoea yenye madhara.—Met 14:23; 20:1; 2Ko 7:1.
Amewaingiza katika undugu wa Kikristo wenye upendo.—Yoh 13:35; 1Yo 3:17, 18.
Anawapa tumaini.—Zb 9:18; Isa 65:21-23.
Hata hali yetu iwe mbaya kadiri gani, hatuna sababu ya kuhangaika. (Isa 30:15) Yehova atashughulikia mahitaji yetu ya kimwili maadamu tunaendelea kutafuta kwanza Ufalme wake.—Mt 6:31-33.
TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA UPENDO HAUSHINDWI KAMWE LICHA YA . . . UMASKINI—KONGO, KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:
Ndugu wanaoishi karibu na mahali ambapo kusanyiko la eneo litafanyiwa, wamewaonyeshaje ukarimu ndugu ambao lazima wasafiri kuhudhuria kusanyiko?
Video hiyo inafundisha nini kuhusu upendo ambao Yehova anawaonyesha maskini?
Hata iwe tuna hali gani ya kiuchumi, tunaweza kumwigaje Yehova?