Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 10/07 uku. 1
  • Wape Maskini Tumaini

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wape Maskini Tumaini
  • Huduma ya Ufalme—2007
  • Habari Zinazolingana
  • Karibuni, Hakuna Atakayekuwa Maskini!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Fuata Kielelezo Cha Yesu Kwa Kuwahangaikia Maskini
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
  • Umaskini Unaoongezeka—Tisho kwa Wote
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
  • Mwisho wa Umaskini Wakaribia
    Amkeni!—1998
Pata Habari Zaidi
Huduma ya Ufalme—2007
km 10/07 uku. 1

Wape Maskini Tumaini

1 Yesu aliwaonyesha maskini upendezi wa pekee. Kuna nyakati ambazo aliwapa msaada wa kimwili na kuwaponya kimuujiza, lakini alikazia fikira kuwatangazia maskini “habari njema.” (Mt. 11:5) Leo, huduma ya Kikristo inaendelea kuwaletea maskini faida na watu wengine vilevile.—Mt. 24:14; 28:19, 20.

2 Tumaini Hakika: Mara nyingi, wahudumu wa dini zinazodai kuwa za Kikristo huwaahidi maskini kwamba watafanikiwa sana wakitoa kwa ukarimu mali zao kanisani. Hata hivyo, Biblia inafundisha kwamba ni Ufalme wa Mungu tu utakaokomesha umaskini na kutatua matatizo yote ya wanadamu. (Zab. 9:18; 145:16; Isa. 65:21-23) Kwa kuwaonyesha maskini kile ambacho Biblia inafundisha hasa, tunawapa tumaini na tunawasaidia kutosheleza uhitaji wao wa kiroho.—Mt. 5:3.

3 Mafarisayo wa siku za Yesu waliwadharau maskini, wakiwaita ‘am-ha·’aʹrets, au “watu wa ardhi.” Hata hivyo, Yesu aliona “damu yao,” au uhai wao, kuwa kitu chenye “thamani.” (Zab. 72:13, 14) Tunaweza kumwiga Yesu na ‘kuwaonyesha maskini kibali’ kwa kuwa wenye fadhili na huruma. (Met. 14:31) Hatungependa kuzungumza kwa dharau kuhusu watu wanaoishi katika maeneo yenye umaskini au kuonyesha kwamba hatutaki kuwahubiria. Wengi ambao wanaitikia ujumbe wa Ufalme ni watu maskini.

4 Wasaidie Sasa: Pia, kuwafundisha maskini walio katika eneo letu kanuni za Biblia huwasaidia kupunguza madhara ya umaskini sasa hivi. Kwa mfano, Biblia hushutumu ulevi, kucheza kamari, uvivu, matumizi ya tumbaku, na mazoea mengine yanayochangia umaskini. (Met. 6:10, 11; 23:21; 2 Kor. 7:1; Efe. 5:5) Maandiko yanawatia watu moyo wawe wanyoofu na wafanye kazi “kwa nafsi yote,” sifa ambazo wafanyakazi wanatazamiwa wawe nazo. (Kol. 3:22, 23; Ebr. 13:18) Kwa kweli, katika uchunguzi mmoja waajiri wengi walisema kwamba unyoofu na uaminifu ndizo sifa zinazowapendeza zaidi kati ya watu wanaotafuta kazi.

5 Yehova anajali sana maskini wanapoteseka. Hivi karibuni Yesu Kristo atamkomboa “maskini anayelilia msaada.” (Zab. 72:12) Hadi wakati huo, tuna pendeleo la kuwafariji wengine, kutia ndani maskini, kwa ujumbe wa tumaini wa Biblia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki