MAISHA YA MKRISTO
Kampeni ya Pekee ya Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Mwezi Septemba
Katika mwezi wa Septemba tutafanya kazi kwa bidii ili kuwaalika watu katika kila familia wajifunze Biblia kwa kutumia broshua Furahia Maisha Milele! Wahubiri wanaweza kufanya upainia msaidizi kwa kutimiza takwa la saa 30. Tunawezaje kushiriki katika kampeni hii ya pekee?
Katika Ziara ya Kwanza: Tumia ukurasa wa nyuma wa broshua ili kuchochea upendezi na kuonyesha jinsi tunavyoongoza funzo la Biblia. Kumbuka wale walionyesha upendezi hapo awali, kutia ndani watu ambao umewahi kuwarudia. Hata ikiwa walikataa kujifunza hapo awali, huenda wakapenda njia yetu mpya ya kujifunza na broshua yetu mpya. Hatupaswi kuacha broshua kwenye nyumba ambayo hatupati mtu au kuzitia kwenye barua tunazowatumia watu ambao hawajaonyesha upendezi. Halmashauri ya Utumishi ya Kutaniko inaweza kupanga mikutano mingi zaidi ya utumishi katika mwezi wa Septemba.
Fursa Nyingine: Ikiwa kutaniko lenu linafanya mahubiri kwa kutumia kigari, basi mnaweza kuweka broshua Furahia Maisha Milele! Waeleze wale wanaoonyesha upendezi kwamba baada ya kupata broshua, wanaweza pia kupata funzo la Biblia bila malipo. Waonyeshe kifupi jinsi tunavyofanya funzo la Biblia, au upange kuwaonyesha baadaye. Mwangalizi wa utumishi anaweza kupanga wahubiri wenye uzoefu waende kwenye biashara zilizo katika eneo na kuwaalika watu wajifunze Biblia. Unaweza pia kuwaalika watu unaokutana nao unapohubiri isivyo rasmi, na pia wale unaofanya nao kazi.
Yesu alituamuru ‘tukafanye wanafunzi,’ na “kuwafundisha.” (Mt 28:19, 20) Tunatumaini kampeni hii ya pekee itatusaidia kutimiza lengo hilo tunapotumia Furahia Maisha Milele!