MAISHA YA MKRISTO
Kabiliana na Matatizo ya Kiuchumi kwa Uhakika
Maisha ya siku za mwisho yamejaa matatizo. Kadiri tunavyokaribia mwisho wa mfumo huu wa mambo, kwa hakika matatizo yataongezeka. Huenda tukapungukiwa na vitu vya kimwili. (Hab 3:16-18) Ni nini kitakachotusaidia kukabiliana na matatizo ya kiuchumi kwa uhakika? Tunapaswa kuendelea kumtumaini Mungu wetu, Yehova. Ameahidi kuwatunza watumishi wake, naye anaweza kutuandalia mahitaji yetu chini ya hali zozote.—Zb 37:18, 19; Ebr 13:5, 6.
Mambo unayoweza kufanya:
Msihi Yehova akupe mwongozo, hekima, na utegemezo.—Zb 62:8.
Uwe tayari kukubali kazi ambayo huenda hujawahi kufanya tena.—g 1/10 8-9, masanduku
Dumisha ratiba nzuri ya kiroho, kutia ndani kusoma Neno la Mungu kila siku, kuhudhuria mikutano ya kutaniko, na kushiriki katika huduma
TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA JENGA NYUMBA ITAKAYODUMU—‘RIDHIKA NA VITU VYA SASA,’ KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:
Familia fulani zimekabili matatizo gani?
Ni jambo gani muhimu zaidi maishani?
Tunaweza kuwasaidiaje wale wanaokabili matatizo ya kiuchumi?