Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mwbr24 Julai kur. 1-2
  • Marejeo ya “Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Marejeo ya “Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha”
  • Marejeo ya Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha—2024
  • Vichwa vidogo
  • JULAI 8-14
  • Mnara
  • Hema
  • JULAI 29–AGOSTI 4
  • AGOSTI 5-11
  • Efrati
  • AGOSTI 12-18
Marejeo ya Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha—2024
mwbr24 Julai kur. 1-2

Marejeo ya Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha

JULAI 8-14

HAZINA ZA NENO LA MUNGU ZABURI 60-62

Yehova Anatulinda na Kutuimarisha

it-2 1118 ¶7

Mnara

Matumizi ya Mfano. Wale wanaomtegemea Yehova wakiwa na imani na utii wanapata ulinzi mwingi, kama Daudi alivyoimba: “Wewe [Yehova] ni kimbilio langu, mnara ulio imara unaonilinda dhidi ya adui.” (Zb 61:3) Wanaotambua maana ya jina lake, na wale wanaolitegemea na kuliwakilisha jina hilo kwa uaminifu, hawana lolote la kuogopa: “Jina la Yehova ni mnara wenye nguvu. Mwadilifu hukimbilia humo na kupata ulinzi.”​—Met 18:10; linganisha 1Sa 17:45-47.

it-2 1084 ¶8

Hema

“Hema” lilitimiza kusudi lingine kwa njia ya mfano katika visa fulani. Hema la mtu lilikuwa mahali pa kupumzikia na pa ulinzi kutokana na hali ya hewa. (Mwa 18:1) Kupatana na desturi za ukaribishaji-wageni, wageni waliamini kwamba wangetunzwa na kuheshimiwa walipokaribishwa katika hema la mtu. Kwa msingi huo, Ufunuo 7:15 inapozungumza kuhusu umati mkubwa na kusema kwamba Mungu “atatandaza hema lake juu yao,” inadokeza kwamba atawaandalia utunzaji wenye ulinzi na usalama. (Zb 61:3, 4) Isaya alitaja kuhusu maandalizi ambayo mke wa Mungu, yaani Sayuni, angefanya kwa ajili ya wana ambao angezaa. Aliambiwa apafanye “mahali pa hema [lake] pawe na nafasi kubwa zaidi.” (Isa 54:2) Hivyo, alipanua eneo la ulinzi kwa ajili ya watoto wake.

JULAI 29–AGOSTI 4

HAZINA ZA NENO LA MUNGU ZABURI 69

Matukio Katika Maisha ya Yesu Yalitabiriwa Kwenye Zaburi 69

it-2 650

Mmea Wenye Sumu

Kumhusu Masihi, ilitabiriwa kwamba angepewa “mmea wenye sumu” kuwa chakula. (Zb 69:21, maelezo ya chini) Hilo lilitokea wakati ambapo Yesu Kristo alipewa divai iliyochanganywa na nyongo kabla ya kutundikwa mtini, lakini alipoionja, akakataa kunywa kinywaji hicho kinacholewesha ambacho huenda kilikusudiwa kumpunguzia mateso yake. Alipoandika utimizo wa unabii huo, Mathayo (27:34) alitumia neno la Kigiriki kho·leʹ (nyongo), neno lilelile linalotumiwa katika Septuajinti ya Kigiriki kwenye Zaburi 69:21. Hata hivyo, simulizi katika Injili ya Marko linataja manemane (Mk 15:23), na hilo limetokeza wazo kwamba katika kisa hiki “mmea wenye sumu” au “nyongo” ulikuwa “manemane.” Uwezekano mwingine ni kwamba kinywaji hicho kinacholewesha kilitia ndani vitu vyote viwili, nyongo na manemane.

AGOSTI 5-11

HAZINA ZA NENO LA MUNGU ZABURI 70-72

Hazina za Kiroho

it-1 768

Efrati

Mpaka wa Eneo Ambalo Waisraeli Walipewa na Mungu. Mungu alipozungumza na Abrahamu, alifanya agano kwamba atawapa wazao wa Abrahamu nchi “kuanzia mto wa Misri mpaka kwenye ule mto mkubwa, mto Efrati.” (Mwa 15:18) Ahadi hiyo ilirudiwa kwa taifa la Israeli. (Kut 23:31; Kum 1:7, 8; 11:24; Yos 1:4) Kitabu cha Kwanza cha Mambo ya Nyakati 5:9 kinasema kwamba kabla ya utawala wa Daudi, wazao fulani wa Rubeni walipanua eneo lao “mpaka mahali ambapo nyika inaanzia kwenye Mto Efrati.” Hata hivyo, kwa kuwa Mto Efrati uko umbali wa kilomita 800 “upande wa mashariki wa Gileadi” (1Nya 5:10), huenda hilo lilimaanisha tu kwamba Warubeni walipanua eneo lao kuelekea Mashariki ya Gileadi kufikia ukingo wa Jangwa la Siria, ambalo lilienea hata kupita Mto Efrati. (BHN inasema, “hadi kwenye maingilio ya jangwa lililoenea hadi mto Eufrate”; RSUVDC, “hadi mwanzoni mwa jangwa litokalo mto wa Frati.”) Hivyo inaonekana kwamba ahadi ya Yehova ilitimizwa kikamili kwa mara ya kwanza wakati wa utawala wa Daudi na wa Sulemani wakati ambapo mipaka ya utawala wa Israeli ilipanuka ikatia ndani ufalme wa Soba wa Waaramu na hivyo ukafika kwenye kingo za Efrati, kwenye sehemu iliyokuwa Siria kaskazini. (2Sa 8:3; 1Fa 4:21; 1Nya 18:3-8; 2Nya 9:26) Kwa sababu ya umuhimu wake, mara nyingi Efrati ulirejelewa tu kama “Mto.”​—Yos 24:2, 15; Zb 72:8.

AGOSTI 12-18

HAZINA ZA NENO LA MUNGU ZABURI 73-74

Hazina za Kiroho

it-2 240

Lewiathani

Zaburi 74 inafafanua rekodi ya Mungu ya kuwaokoa watu wake, na mstari wa 13 na 14 zinarejelea kwa njia ya mfano jinsi alivyolikomboa taifa la Israeli kutoka Misri. Hapo maneno “wanyama wakubwa sana wa baharini [Kiebrania, than·ni·nimʹ, wingi wa tan·ninʹ]” yanatumiwa wakati uleule kurejelea “Lewiathani,” na huenda maneno kuponda vichwa vya Lewiathani yakamaanisha ushindi dhidi ya Farao na jeshi lake wakati wa Kutoka Misri. Hapa Targum za Kiaramu zinasema “wenye nguvu wa Farao” badala ya “vichwa vya Lewiathani.” (Linganisha Eze 29:3-5, ambapo Farao anafananishwa na “mnyama mkubwa sana wa baharini” anayelala kati ya vijito vya mto Nile; pia Eze 32:2.) Inaonekana kwamba Isaya 27:1 inataja Lewiathani (LXX, “joka”) kama mfano wa milki, shirika ambalo lina uvutano wa kimataifa na linalodhibitiwa na mtu ambaye anarejelewa kuwa “joka.” (Ufu 12:9) Huo ni mmoja kati ya unabii mwingi wa kurudishwa kwa taifa la Israeli, kwa hiyo, inaposema kwamba Yehova “atamwelekezea fikira” Lewiathani, lazima Babiloni liwe linatiwa ndani. Hata hivyo, mstari wa 12 na 13 unatia ndani pia Ashuru na Misri. Hivyo, inaonekana kwamba hapa Lewiathani anarejelea shirika la kimataifa au milki inayompinga Yehova na waabudu wake.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki