Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • wp21 Na. 2 kur. 7-9
  • Yesu Alisema Mwisho Utakuja Lini?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Yesu Alisema Mwisho Utakuja Lini?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2021
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • FIKIRIA MAMBO MAWILI AMBAYO YESU ALISEMA KUHUSU MWISHO:
  • ISHARA
  • “SIKU ZA MWISHO”
  • DUNIA PARADISO IKO KARIBU!
  • Maswali Manne Kuhusu Mwisho Yajibiwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
  • Je, Tunaishi Katika “Siku za Mwisho”?
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
  • Karibuni Kusudi la Mungu Kutimizwa
    Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai?
  • Je, Mwisho wa Dunia Uko Karibu?
    Biblia Inatufundisha Nini?
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2021
wp21 Na. 2 kur. 7-9
Yesu akiwafafanulia mitume wake ishara ya siku za mwisho.

Yesu Alisema Mwisho Utakuja Lini?

Kama tulivyojifunza kwenye makala iliyopita, Biblia inapozungumzia mwisho wa ulimwengu haimaanishi mwisho wa sayari yetu dunia au wa wanadamu. Badala yake, inamaanisha mwisho wa mfumo huu mwovu wa mambo na wale wote wanaouunga mkono. Hata hivyo, Biblia inasema mwisho utakuja lini?

FIKIRIA MAMBO MAWILI AMBAYO YESU ALISEMA KUHUSU MWISHO:

“Kwa hiyo, endeleeni kukesha kwa sababu hamjui ile siku wala saa.”​—MATHAYO 25:13.

“Endeleeni kutazama, endeleeni kukaa macho, kwa maana hamjui wakati uliowekwa ni lini.”​—MARKO 13:33.

Kwa hiyo, hakuna mtu yeyote duniani anayejua kihususa mwisho utakuja lini. Lakini, Mungu ameweka wakati hususa, yaani, “siku na saa” ya mwisho wa ulimwengu. (Mathayo 24:36) Je, hilo linamaanisha hakuna kabisa njia yoyote ya kujua ikiwa mwisho uko karibu? La hasha. Yesu aliwaambia wanafunzi wake wawe macho kuona baadhi ya matukio ambayo yangeashiria kuwa mwisho uko karibu.

ISHARA

Yesu alitaja matukio ambayo yangekuwa ishara ya “umalizio wa mfumo wa mambo.” Alisema hivi: “Taifa litapigana na taifa na ufalme kupigana na ufalme, kutakuwa na upungufu wa chakula na matetemeko ya ardhi sehemu mbalimbali.” (Mathayo 24:3, 7) Pia, alisema kutakuwa na “magonjwa,” yaani, magonjwa yanayosambaa kwa kasi. (Luka 21:11) Je, unajionea mambo hayo ambayo Yesu alitabiri?

Leo, watu wanateseka sana kwa sababu ya vita, njaa, matetemeko ya ardhi, na magonjwa mbalimbali. Kwa mfano, mwaka wa 2004, tetemeko kubwa la ardhi lililotokea kwenye bahari ya Hindi lilisababisha tsunami iliyoua watu 225,000 hivi. Katika kipindi cha miaka mitatu, ugonjwa wa corona (COVID-19) umesababisha vifo vya watu milioni 6.9 hivi duniani pote. Yesu alisema matukio kama hayo yangeonyesha kwamba mwisho wa ulimwengu uko karibu.

“SIKU ZA MWISHO”

Biblia inakiita “siku za mwisho,” kipindi kifupi cha wakati kabla ya mwisho wa ulimwengu. (2 Petro 3:3, 4) Timotheo ya pili 3:1-5 inasema kwamba siku za mwisho zingetambuliwa kwa kuporomoka kwa maadili. (Ona sanduku lenye kichwa; “Kabla ya Mwisho wa Ulimwengu.”) Je, unajionea watu wakiwa wabinafsi, wenye pupa, wakali, na wasio na upendo? Jambo hilo pia ni uthibitisho kwamba tunaishi karibu zaidi na mwisho wa ulimwengu.

Siku za mwisho zitadumu kwa muda gani? Kulingana na Biblia, kitakuwa “kipindi kifupi cha wakati.” Kisha, Mungu atawaharibu “wale wanaoiharibu dunia.”​—Ufunuo 11:15-18; 12:12.

Vita

Wanajeshi walio vitani wakifyatua risasi wakiwa nyuma ya ukuta wa kujilinda.
  • Kati ya mwaka 2007 na 2017, vifo vilivyotokana na mashambulizi ya kutumia silaha na ugaidi viliongezeka kwa asilimia 118

Magonjwa

Mgonjwa akiwa amelala kwenye kitanda cha hospitali.
  • Magonjwa yanayoongoza kwa kuua watu wengi ni ugonjwa wa moyo, kiharusi, ugonjwa wa mapafu, magonjwa yanayotokana na uzazi, kuharisha, kansa, kifua kikuu

Njaa

Msichana mwenye njaa ameshika bakuli.
  • Katika mwaka wa 2021, asilimia 9.8 ya watu wote duniani walikabiliwa na janga la njaa na mmoja kati ya watoto watatu walio chini ya umri wa miaka mitano walikuwa na utapiamlo na kudumaa

Kazi ya Kuhubiri Ulimwenguni Pote

Mashahidi wa Yehova wakiwa wamesimama pembeni ya kigari cha machapisho wakizungumza na mwanamume mmoja.
  • Mashahidi wa Yehova zaidi ya milioni 8.6 duniani pote wanasambaza machapisho ya Biblia kwenye nchi 240 katika lugha zaidi ya 1000

DUNIA PARADISO IKO KARIBU!

Tayari Mungu ameweka siku na saa ya kuuangamiza mfumo huu mwovu wa mambo. (Mathayo 24:36) Hata hivyo, kuna habari nyingine njema—Mungu “hataki yeyote aangamizwe.” (2 Petro 3:9) Kwa sasa, anawapa wanadamu nafasi ya kuishi kulingana na viwango vyake. Kwa nini? Kwa sababu anataka tuokoke mwisho wa ulimwengu huu na kuishi katika dunia itakayokuwa paradiso.

Mungu amepanga programu ya elimu ya Biblia ulimwenguni pote inayowasaidia watu kujua mambo ya kufanya ili waishi katika ulimwengu mpya chini ya Ufalme wake. Yesu alisema habari njema ya Ufalme wa Mungu ingehubiriwa “katika dunia yote inayokaliwa.” (Mathayo 24:14) Mashahidi wa Yehova ulimwenguni pote walitumia mabilioni ya saa kuwahubiria na kuwafundisha watu ujumbe wa tumaini wa Biblia. Yesu alisema kwamba kazi hii ya kuhubiri ingefanywa duniani kote kabla ya mwisho kuja.

Muda wa utawala wa wanadamu unakaribia kwisha. Lakini habari njema ni kwamba, unaweza kuokoka mwisho wa ulimwengu huu na kuishi katika dunia Paradiso ambayo Mungu ameahidi. Makala inayofuata itazungumzia mambo unayoweza kufanya ili uishi katika ulimwengu huo mpya.

KABLA YA MWISHO WA ULIMWENGU

“Katika siku za mwisho kutakuwa na nyakati za hatari zilizo ngumu kushughulika nazo. Kwa maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda pesa, wenye kujidai, wenye majivuno, wakufuru, wasiotii wazazi, wasio na shukrani, wasio washikamanifu, wasio na upendo wa asili, wasiotaka makubaliano yoyote, wachongezi, wasiojizuia, wakali, wasiopenda wema, wasaliti, wenye vichwa vigumu, waliojaa kiburi, wanaopenda raha badala ya kumpenda Mungu, wakionekana kama watu wanaomwogopa Mungu lakini wakizikana nguvu zake.”​—2 TIMOTHEO 3:1-5.

Unabii wa Yesu kuhusu “siku za mwisho” unatupatia sababu ya kuwa na tumaini

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki