Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • wp21 Na. 2 kur. 10-12
  • Mambo Unayoweza Kufanya Ili Uishi Katika Ulimwengu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mambo Unayoweza Kufanya Ili Uishi Katika Ulimwengu Mpya
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2021
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • UKIMJUA MUNGU UTAOKOLEWA MWISHO WA ULIMWENGU HUU UTAKAPOKUJA
  • SOMA NENO LA MUNGU, BIBLIA, KILA SIKU
  • MWOMBE MUNGU MSAADA
  • Mungu Amefanya Mambo Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu Wote)—2019
  • Unapaswa Kufanya Nini Ili Uishi Milele?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Njia ya Kuishi Milele
    Kumsikiliza Mwalimu Mkuu
  • Unaweza kuishi katika ulimwengu mpya wa Mungu Wenye Amani
    Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2021
wp21 Na. 2 kur. 10-12

Mambo Unayoweza Kufanya Ili Uishi Katika Ulimwengu Mpya

Katika makala zilizotangulia tulijifunza kwamba hivi karibuni Mungu atawaangamiza wanadamu wote waovu na kuondoa matatizo yote. Tuna uhakika kwamba jambo hilo litatokea. Kwa nini? Kwa sababu Neno la Mungu, Biblia, limeahidi hivi:

“Ulimwengu unapitilia mbali.”​—1 YOHANA 2:17.

Tunaweza kuwa na uhakika kwamba baadhi ya watu wataokolewa kwa sababu mstari huohuo unaahidi hivi:

“Yule anayefanya mapenzi ya Mungu anadumu milele.”

Hivyo, ili tuweze kuokolewa tunapaswa kufanya mapenzi ya Mungu. Na ili tujue mapenzi ya Mungu, kwanza, tunahitaji kumjua vizuri.

UKIMJUA MUNGU UTAOKOLEWA MWISHO WA ULIMWENGU HUU UTAKAPOKUJA

Picha: 1. Muuguzi amekaa kwenye sakafu, akiwa amechoka na kuvunjika moyo. 2. Akiwa amepumzika mkahawani, anamwona mfanyakazi mwenzake akifurahia kusoma gazeti. 3. Mfanyakazi mwenzake anamsomea mstari wa Biblia na kumpatia kadi ya mawasiliano ya jw.org.

Yesu alisema: “Uzima wa milele ndio huu, wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli.” (Yohana 17:3) Ili tuokolewe na kuishi milele, tunahitaji kumjua Mungu. Hilo linatia ndani mambo mengi zaidi ya kujua tu Mungu yupo au kujua mambo machache kumhusu. Tunahitaji kuwa marafiki wa Mungu. Ili urafiki wowote uimarike na kusitawi, tunahitaji kutumia muda pamoja na marafiki wetu. Hivyo ndivyo tunavyopaswa kufanya inapohusu urafiki wetu na Mungu. Fikiria kweli muhimu tunazojifunza kutoka katika Biblia zinazotusaidia kusitawisha na kudumisha urafiki wetu na Mungu.

Kweli Tunazojifunza Kutoka Kwenye Biblia

Muuguzi akitazama tovuti ya jw.org akiwa nyumbani kwake.

Tunajifunza kwamba Mungu alikusudia tuishi kwenye Paradiso.

Aliwaumba wanadamu wa kwanza, Adamu na Hawa, na kuwaweka kwenye bustani maridadi iliyoitwa Edeni. Walikuwa wakamilifu, na Mungu aliwapa kila kitu walichohitaji ili wafurahie maisha. Wangeweza kuishi milele. Ikiwa wangedumisha urafiki wao na Mungu, hawangekufa kamwe. Lakini walichagua kutotii amri rahisi waliyopewa na Mungu.

Tunajifunza kwa nini tunateseka sana leo.

Kwa kutomtii Mungu, mwanadamu wa kwanza, Adamu, alijipotezea nafasi ya kuishi milele na akafanya wanadamu wote wapoteze nafasi hiyo. Biblia inasema hivi: “Kupitia mtu mmoja dhambi iliingia katika ulimwengu na kifo kupitia dhambi, basi kifo kikaenea kwa watu wote.” (Waroma 5:12) Kama vile mtoto anavyoweza kurithi ugonjwa kutoka kwa wazazi wake, ndivyo watoto wote wa Adamu walivyorithi kutokamilika kutoka kwake. Ndiyo sababu tunazeeka na kufa.

Tunajifunza kwamba tayari Mungu amefanya mipango ili kutusaidia.

Biblia inasema hivi: “Mungu aliupenda ulimwengu sana hivi kwamba akamtoa Mwana wake mzaliwa pekee, ili kila mtu anayemwamini asiangamizwe bali awe na uzima wa milele.” (Yohana 3:16) Mungu alimtuma Yesu duniani ili atoe uhai wake kwa ajili yetu. Alipokuwa akizungumzia jambo hilo, Prabhakar, mwanamume mwenye umri wa miaka 86 kutoka India, alisema hivi: “Jambo hilo linanithibitishia kwamba Yehovaa ananipenda sana. Upendo wake umenipatia tumaini la kuishi milele.”

Tunajifunza jinsi ya kuonyesha shukrani kwa mambo ambayo Mungu ametufanyia.

Biblia inasema tunaweza kuonyesha shukrani kwa mambo ambayo Mungu ametufanyia kwa “kuzishika amri zake.” (1 Yohana 2:3) Kwa upendo, Yehova Mungu anatuambia mambo tunayoweza kufanya ili tufurahie maisha sasa. (Isaya 48:17, 18, maelezo ya chini) Mungu hataki tuteseke. Anaahidi ikiwa tutafuata mwongozo wake, tutafurahia maisha sasa na pia tutapata nafasi ya kuishi milele.

SOMA NENO LA MUNGU, BIBLIA, KILA SIKU

Muuguzi akitazama mbinguni baada ya kusoma Biblia wakati wa mapumziko ya mchana.

Unaweza kuokoka mwisho wa ulimwengu huu kwa kumwomba Mungu msaada na kufanya mapenzi yake

Tunakula chakula kila siku ili tuendelee kuishi. Lakini Yesu alisema hivi: “Mwanadamu hataishi kwa mkate tu, bali kwa kila neno linalotoka katika kinywa cha Yehova.”​—Mathayo 4:4.

Leo, tunapata maneno ya Yehova kwenye Biblia. Unapojifunza kitabu hiki kitakatifu, utaelewa mambo ambayo Mungu alifanya zamani, anayofanya sasa, na atakayofanya wakati ujao.

MWOMBE MUNGU MSAADA

Tunaweza kufanya nini ikiwa tunataka kufuata mwongozo wa Mungu lakini ni vigumu kwetu kuacha mambo ambayo Mungu anasema ni mabaya? Katika hali kama hiyo, kumjua Mungu vizuri kunaweza kutusaidia.

Mfikirie mwanamke tutakayemwita Sakura ambaye zamani aliishi maisha mapotovu. Alipoanza kujifunza Biblia, alijifunza kuhusu amri ya Mungu ya ‘kuukimbia uasherati.’ (1 Wakorintho 6:18) Sakura alisali ili Mungu amsaidie na aliweza kuacha zoea hilo baya. Hata hivyo, bado anahitaji kupambana na vishawishi. Anasema hivi: “Ikiwa ninaanza kuwaza mambo mapotovu, ninasali kwa Yehova kutoka moyoni, nikijua kwamba siwezi kupambana na hali hiyo peke yangu. Kusali kumenifanya niwe karibu zaidi na Yehova.” Kama Sakura, mamilioni ya watu wanaendelea kupata ujuzi kumhusu Mungu. Anawapa nguvu wanazohitaji ili wafanye mabadiliko katika maisha yao na kuishi kwa njia inayompendeza Yeye.​—Wafilipi 4:13.

Kadiri unavyoendelea kumjua Mungu vizuri, ndivyo atakavyokujua wewe kama rafiki yake mpendwa. (Wagalatia 4:9; Zaburi 25:14) Kisha, utaweza kuokolewa na kuingia katika ulimwengu mpya wa Mungu. Lakini, ulimwengu mpya utakuwaje? Makala inayofuata itazungumzia jambo hilo.

a Yehova ni jina la Mungu kama linavyoonyeshwa kwenye Biblia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki