Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w24 Oktoba uku. 32
  • Pitia Mambo Makuu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Pitia Mambo Makuu
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2024
  • Habari Zinazolingana
  • Kukazia Mambo Makuu
    Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
  • Kukazia Mambo Makuu
    Boresha Uwezo Wako wa Kusoma na Kufundisha
  • Kutayarisha Muhtasari
    Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
  • Sehemu ya 2: Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo
    Huduma Yetu ya Ufalme—2004
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2024
w24 Oktoba uku. 32

DOKEZO LA KUJIFUNZA

Pitia Mambo Makuu

Je, nyakati nyingine ni vigumu kwako kukumbuka mambo ambayo umetoka tu kujifunza? Jambo hilo linatupata sisi sote pindi fulani. Ni nini kinachoweza kutusaidia? Kupitia mambo makuu.

Unapojifunza, tua mara kwa mara na ufikirie mambo makuu. Ona jinsi mtume Paulo alivyowasaidia wale waliokuwa wakichunguza barua yake wafanye hivyo, aliandika hivi: “Sasa jambo kuu tunalosema ni hili.” (Ebr. 8:1) Akitumia maneno hayo, aliwasaidia wasikilizaji wake wafuatane vizuri na habari aliyozungumzia na kutambua jinsi kila wazo lilivyohusiana na jambo kuu.

Huenda ukatenga wakati, labda dakika kumi mwishoni mwa kila kipindi cha funzo, ili utafakari kuhusu mawazo makuu ya mambo ambayo umejifunza. Ikiwa hukumbuki, angalia vichwa vidogo au sentensi inayobeba wazo kuu—mara nyingi inakuwa sentensi ya kwanza katika kila fungu—ili kujikumbusha. Ikiwa umejifunza jambo fulani jipya, jaribu kulielezea kwa maneno yako mwenyewe. Unapopitia mambo makuu, hilo litakusaidia kukumbuka na pia kuelewa zaidi jinsi unavyoweza kuitumia habari hiyo maishani.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki