Utendaji wa Mashahidi wa Yehova Katika Nyakati za Kisasa
Urusi
Masimulizi ya imani na ujasiri wa Mashahidi wa Yehova nchini Urusi na masimulizi ya uaminifu wao kwa Mungu licha ya upinzani mkali na usiokoma. Kupelekwa uhamishoni, vifungo, na kambi za kazi ngumu, mambo yote hayo hayangeweza kuwanyamazisha Mashahidi au kuvunja msimamo wao.
Masimulizi hayo hayahuzunishi. Wale walioweka imani yao kwa Yehova hawakujisikitikia. Walitarajia wangeteswa na waliona hiyo kuwa fursa ya kuthibitisha uaminifu wao kwa Mungu. Ndugu mmoja alisema hivi: “Hukumu ilipokuwa ikisomwa, hakuna yeyote kati ya wanafunzi wangu wa Biblia aliyeingiwa na hofu. Nilifurahia sana jambo hilo. Wote wanne walihukumiwa kifungo cha miaka 25 kwenye kambi. Nilipewa hukumu kali zaidi . . . Tulisimama ili kumshukuru Yehova kwa kututegemeza. Walinzi walishtuka na kushangaa ni kwa nini tulikuwa na furaha hivyo.”
Soma kuhusu msichana aliyepata kweli kutokana na barua zilizofungwa kwenye jiwe na kutupwa nje ya ua wa seng’enge wa gereza. Soma jinsi ndugu waliokuwa gerezani walivyojiimarisha kiroho. Ona kile kilichotukia baada ya wazazi Mashahidi kulaumiwa isivyo haki kwamba walikata sikio la binti yao.
Makumi ya miaka chini ya marufuku ni sehemu moja ya masimulizi hayo. Katika miaka 20 ambayo imepita, idadi ya Mashahidi imeongezeka kwa njia ya ajabu kotekote katika nchi hiyo. Ona jinsi ambavyo ndugu walikabiliana na jinsi ambavyo walishinda vipingamizi vilivyoletwa na ukuzi huo mkubwa. Tunafurahi kutumia sehemu yote ya kihistoria ya Kitabu cha Mwaka kuzungumzia nchi moja tu, yaani, Urusi.