Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • yb12 kur. 3-5
  • Barua Kutoka kwa Baraza Linaloongoza

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Barua Kutoka kwa Baraza Linaloongoza
  • 2012 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
  • Habari Zinazolingana
  • Barua Kutoka kwa Baraza Linaloongoza
    2009 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
  • Matukio Muhimu ya Mwaka Uliopita
    2012 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
  • Barua Kutoka Kwa Baraza Linaloongoza
    2004 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehovah
  • Barua Kutoka kwa Baraza Linaloongoza
    2014 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehovah
Pata Habari Zaidi
2012 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
yb12 kur. 3-5

Barua Kutoka kwa Baraza Linaloongoza

Ndugu Zetu Wapendwa:

Tunafurahi sana kuwaandikia ninyi watumishi waaminifu wa Yehova, ambao kwa sasa idadi yenu ni zaidi ya milioni saba. Unapokutana na mwamini mwenzako kutoka sehemu nyingine ya dunia, mara moja unahisi upendo wa pekee kumwelekea. (Yoh. 13:34, 35) Bila shaka, utahisi upendo huo wa pekee tena unaposoma hiki Kitabu cha Mwaka kilicho na masimulizi kuhusu imani na ushikamanifu wa ndugu na dada kutoka nchi mbalimbali.

Ripoti kutoka ulimwenguni pote inaonyesha kwamba wengi wenu mnachukulia kwa uzito mpango wa Ibada ya Familia. Ninyi mlio na watoto wadogo mmevumbua njia nyingi za kuvuta uangalifu wa watoto wenu. (Efe. 6:4) Wenzi wa ndoa wanaimarisha uhusiano wao wanapojifunza pamoja. (Efe. 5:28-33) Kwa kweli, watu mmoja-mmoja na wale walio na familia wananufaika kupitia mpango huo wa kujifunza Neno la Mungu kwa undani.—Yos. 1:8, 9.

Tunahuzunika pamoja nanyi nyote mlioathiriwa na misiba ya asili ya hivi karibuni. Tunachukua fursa hii kuwashukuru wengi ambao, bila kusita, wametoa misaada wakati wa taabu. (Mdo. 11:28-30; Gal. 6:9, 10) Vilevile, katika kila kutaniko, kuna wale ambao hutambua mahitaji ya kimwili ya ndugu zetu na kuwasaidia. Kama Dorkasi anayetajwa katika Biblia, mnazidi katika “matendo mema na zawadi za rehema.” (Mdo. 9:36) Muwe na hakika kwamba Yehova anaona na atawalipa vilivyo.—Mt. 6:3, 4.

Katika nchi nyingine, mnanyimwa haki zenu na watu wanaotumia sheria vibaya ili ‘kutunga matatizo kwa njia ya amri.’ (Zab. 94:20-22) Mnatambua kuwa Yesu alitabiri kwamba mateso yangetukia, na hivyo mnavumilia kwa ujasiri huku mkipata kimbilio kwa Yehova. (Yoh. 15:19, 20) Muwe na hakika kwamba tunawataja katika sala, huku mkiendelea “kujitetea mbele ya kila mtu ambaye hutaka kutoka kwenu sababu ya tumaini lililo ndani yenu.”—1 Pet. 3:13-15.

Tunawapongeza nyote ambao mnaendelea kubaki safi kiadili mwaka baada ya mwaka licha ya mbinu zisizo wazi za Shetani za kueneza upotovu wa maadili. Katika nyakati hizi ambazo viwango vya maadili ulimwenguni vinaendelea kushuka hata zaidi, ‘mnajipatia nguvu katika Bwana na katika uwezo wa nguvu zake.’ (Efe. 6:10) ‘Mmevaa mavazi kamili ya silaha kutoka kwa Mungu’ na hivyo mnasimama imara dhidi ya “hila za Ibilisi.” (Efe. 6:11, 12) Jueni kwamba kupitia mfano wenu, Yehova anapata jibu lililo wazi la kumpa Shetani, anayemdhihaki.—Met. 27:11.

Tulifurahi sana kujua kwamba katika mwaka wa 2011, watu 19,374,737 walihudhuria Ukumbusho wa kifo cha Bwana. Kwa kiwango fulani, idadi hiyo ilichangiwa na jitihada za wengi wenu walioitikia mwito wa kuwa mapainia wasaidizi mwezi wa Aprili. Mamilioni ya watu ulimwenguni walisikia Mashahidi washikamanifu wakimsifu Yehova kwa umoja! (Rom. 10:18) Iwe ulikuwa mmoja wa wale 2,657,377 waliotumika wakiwa mapainia wasaidizi mwezi huo au ulijitahidi kuongeza utumishi wako kwa njia fulani, nyote mlitufanya tuwe na shangwe nyingi sana kwa kujitoa kwa hiari na kwa bidii.—Zab. 110:3; Kol. 3:23.

Mwaka uliopita, watu 263,131 walionyesha wakfu wao kwa Yehova. Tunamshukuru Yehova kwa jambo hilo, na tunawashukuru ninyi nyote kwa kujiunga nasi tunapowaalika wengine kwa kusema: “‘Njoo!’ Na yeyote anayesikia na aseme: ‘Njoo!’ Na yeyote anayeona kiu aje; yeyote anayetaka achukue maji ya uzima bure.” (Ufu. 22:17) Hasa baada ya makusanyiko ya wilaya ya 2011 yaliyozungumzia mengi kuhusu Ufalme wa Mungu uliosimamishwa, tunasema kwa hamu nyingi zaidi kuliko wakati mwingine wowote, “Ufalme wa Mungu na uje!” Tunachochewa na uhakikisho wa Yesu, “Ninakuja upesi,” na hivyo tunasema pamoja na mtume Yohana: “Amina! Njoo, Bwana Yesu.”—Ufu. 22:20.

Mnapoendelea kungoja tukio hilo lenye kusisimua, muwe na hakika kwamba tunampenda kila mmoja wenu anayeendelea kuthibitisha kwamba anampenda Yehova kwa “tendo na kweli”!—1 Yoh. 3:18.

Ndugu zenu,

Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki