Andiko la Mwaka wa 2012
“Neno Lako Ni Kweli.”—YOHANA 17:17.
Tunashukuru kama nini kwamba Baba yetu wa mbinguni mwenye upendo ametufunulia kweli! Neno lake linatuonyesha njia bora ya maisha na jinsi tunavyoweza kufaidika kikamili maishani. Linatulinda kutokana na mambo ya ubatili na yenye kudhuru, linatukomboa kutokana na utumwa wa mafundisho ya uwongo ya dini, na kutupa amani ya kweli ya akilini. Linatupa kusudi maishani sasa na kutuandalia tumaini zuri la wakati ujao.
Kweli hutuunganisha na mamilioni ya ndugu zetu duniani kote. Muhimu hata zaidi, kweli ya Biblia hutufundisha kumhusu Yehova na kutuonyesha jinsi tunavyoweza kumkaribia. Tusipuuze kamwe kweli ambazo Yehova ametupa. Na tushangilie katika kweli na kuiruhusu ituongoze katika njia zetu zote.