Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • yb15 uku. 120-uku. 121 fu. 3
  • “Tumaini la Ufalme Si Ndoto”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Tumaini la Ufalme Si Ndoto”
  • 2015 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
  • Habari Zinazolingana
  • Kumtumikia Mungu Nyakati za Magumu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
  • Nilikuwa Mwanasiasa Lakini Sasa Mimi Ni Mkristo
    Amkeni!—2002
  • Imani Yajaribiwa Huko Poland
    Amkeni!—2000
  • Kueneza Mbegu za Ufalme Kila Pindi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
Pata Habari Zaidi
2015 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
yb15 uku. 120-uku. 121 fu. 3

JAMHURI YA DOMINIKA

Tumaini la Ufalme Si Ndoto

Efraín De La Cruz

  • ALIZALIWA 1918

  • ALIBATIZWA 1949

  • HISTORIA FUPI Licha ya kufungwa na kupigwa sana katika magereza saba tofauti, hakuacha azimio lake la kuhubiri habari njema ya Ufalme wa Mungu.

Picha katika ukurasa wa 120

MWAKA wa 1948, mimi, mke wangu Paula, na binti yetu tulianza kuhudhuria mikutano ya Mashahidi wa Yehova katika mji wa Blanco Arriba. Tulitembea kilometa 40 kwenda na kurudi, hata hivyo, hatujawahi kukosa mikutano. Mimi na Paula tulibatizwa Januari 3, 1949.

Miezi sita baadaye, baadhi yetu kutanikoni tulikamatwa na kufungwa miezi mitatu gerezani. Tulilala sakafuni na kupewa mlo mmoja tu kwa siku—ndizi na chai. Tulipoachiliwa huru, viongozi wa serikali walitutishia wakidhani kwamba tungeacha kuhubiri. Lakini tuliporudi nyumbani tulianza kuhudhuria mikutano na kuhubiri kwa siri. Kwa kuwa maofisa wa serikali walikuwa wakituchunguza mara kwa mara, tulikutana kwenye nyumba za watu au kwenye mashamba ya kahawa. Badala ya kukusanyika mahali palepale, baada ya kila mkutano tulitangaza mahali ambapo tungefanyia mkutano utakaofuata. Kila mtu alihubiri peke yake; tulivaa nguo za kazi, na hatukutumia machapisho au Biblia. Hata hivyo, kati ya mwaka wa 1949 na 1959, nilifungwa katika magereza saba tofauti, nikitumikia vifungo vya kati ya miezi mitatu mpaka sita kila kifungo.

Nilipaswa kuwa mwangalifu sana kwa sababu baadhi ya wapelelezi walikuwa watu wangu wa ukoo. Ingawa nililala milimani au mashambani ili kujificha, bado nyakati nyingine nilikamatwa. Wakati fulani nilipokamatwa, nilifungwa katika gereza la La Victoria huko Ciudad Trujillo, lililokuwa na wafungwa 50 hadi 60 katika kila seli. Huko tulipewa milo miwili kwa siku, asubuhi tulipewa uji, na mchana kiasi kidogo cha wali na maharagwe. Kila Shahidi aliwahubiria wafungwa wenzake, na tulifanya mikutano kikawaida kwa kunukuu maandiko tuliyokumbuka na kuzungumzia mambo tuliyojionea katika utumishi wa shambani.

Mara ya mwisho nilipokuwa gerezani, askari mmoja alinipiga kichwani na kwenye mbavu kwa kitako cha bunduki. Ingawa bado nina maumivu kwa sababu ya kupigwa na mateso mengine, majaribu hayo yaliimarisha imani yangu, uvumilivu, na azimio langu la kumtumikia Yehova.

Sasa nina umri wa miaka 96 na ninatumikia nikiwa mtumishi wa huduma kutanikoni. Ijapokuwa siwezi kutembea umbali mrefu, ninakaa mbele ya nyumba yangu na kuwahubiria wapita njia. Tumaini la Ufalme si ndoto kwangu. Ni halisi, na nimekuwa nikihubiri kuuhusu kwa zaidi ya miaka 60. Ulimwengu mpya ni halisi kwangu kama ilivyokuwa siku ya kwanza niliposikia ujumbe wa Ufalme.a

a Efraín De La Cruz alikufa simulizi hili lilipokuwa likiandikwa.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki