Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • yb15 uku. 122-uku. 123 fu. 7
  • “Nitaendelea Kuwa Shahidi wa Yehova”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Nitaendelea Kuwa Shahidi wa Yehova”
  • 2015 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
  • Habari Zinazolingana
  • Nashukuru Licha ya Misiba—Jinsi Biblia Ilivyonisaidia Kuvumilia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Miaka Zaidi ya 50 ya ‘Kuvuka’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • Kumtumikia Mungu Nyakati za Magumu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
  • Kuacha Mengi kwa Ajili ya Kitu Bora Zaidi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
Pata Habari Zaidi
2015 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
yb15 uku. 122-uku. 123 fu. 7

JAMHURI YA DOMINIKA

Nitaendelea Kuwa Shahidi wa Yehova

Ana María (Mary) Glass

  • ALIZALIWA 1935

  • ALIBATIZWA 1956

  • HISTORIA FUPI Kijana Mkatoliki aliyekuwa na bidii ambaye alijifunza kweli ya Biblia na kushinda upinzani kutoka kwa familia, Kanisa, na Serikali.

Picha katika ukurasa wa 122

NILIPENDA sana dini na nilikuwa muumini mwenye bidii wa Kanisa Katoliki. Nilikuwa mwimbaji katika kwaya ya kanisa na niliambatana na makasisi kwenye safari zao za kidini, ambako waliongoza Misa. Kisha, mwaka wa 1955 dada yangu alinieleza kuhusu Paradiso ijayo. Alinipa Biblia, kijitabu “This Good News of the Kingdom,” na kitabu “Let God Be True.” Nilivutiwa sana, kwa hiyo nilimwuliza kasisi ikiwa ningeweza kusoma Biblia. Aliniambia kwamba “ningerukwa na akili,” hata hivyo niliamua kuisoma.

Nilipohamia nyumbani kwa babu yangu huko Boca Chica, kasisi mmoja aliniuliza kwa nini niliacha kwenda kanisani. Nilimwambia nimegundua kwamba mafundisho mengi ya kanisa hayapatani na Biblia. Kasisi huyo alighadhabika sana. “Sikiliza binti,” akafoka, “wewe ni kondoo uliyepotea njia kutoka kwenye kundi langu.”

“Hapana,” nikamjibu, “wewe ndiye umepotea njia kutoka kwenye kundi la Yehova, kwa sababu kondoo ni mali ya Yehova wala si ya mwanadamu yeyote.”

Sikurudi tena kanisani. Nilihamia kwa dada yangu, na nilibatizwa miezi sita tu baada ya kuisikia kweli kwa mara ya kwanza. Bila kukawia, nilianza upainia wa kawaida. Mwaka mmoja baadaye niliolewa na Enrique Glass, aliyekuwa akitumikia akiwa mwangalizi wa mzunguko. Siku moja tulipokuwa tukihubiri katika bustani fulani huko La Romana, polisi walimkamata Enrique. Walipokuwa wakiondoka naye, niliwakimbilia na kuwaambia: “Mimi pia ni Shahidi wa Yehova, nami nilikuwa nahubiri. Kwa nini msinikamate mimi pia?” Lakini hawakutaka kunikamata.

Tayari Enrique alikuwa ametumikia vifungo vya gerezani kwa jumla ya miaka saba na nusu. Wakati huu alihukumiwa kifungo cha miezi 20 gerezani. Nilimtembelea Enrique kila Jumapili. Siku moja kapteni wa gereza aliniuliza, “Umekuja kufanya nini?”

Nikamwambia, “Mume wangu alifungwa kwa sababu yeye ni Shahidi wa Yehova.”

“Wewe bado una umri mdogo na unaweza kuwa na wakati ujao mzuri,” akajibu. “Kwa nini upoteze muda wako na Mashahidi wa Yehova?”

“Mimi pia ni Shahidi wa Yehova,” nikamjibu. “Hata mkiniua mara saba na kunifufua mara saba, nitaendelea kuwa Shahidi wa Yehova.” Alikosa la kusema na kuniamuru niondoke.

Baada ya marufuku kuondolewa, mimi na Enrique tulitumikia kwa miaka kadhaa, mume wangu akiwa mwangalizi wa mzunguko na wilaya. Enrique alikufa Machi 8, 2008. Ninaendelea kutumikia nikiwa painia wa kawaida.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki