Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w74 2/15 kur. 79-80
  • Sababu Waligeuka Wakawa Bora

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Sababu Waligeuka Wakawa Bora
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Habari Zinazolingana
  • Kutumia Mashauri ya Biblia Kunaendeleza Umoja wa Jamaa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • “Umtazame Mtu Mnyofu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
  • “Mungu Hana Upendeleo”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Furaha ya Kutimiziwa Mahitaji ya Kiroho
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
w74 2/15 kur. 79-80

Sababu Waligeuka Wakawa Bora

NYAKATI nyingine watu wanasikika wakisema, ‘Mimi sitaweza wakati wo wote kugeuza njia zangu.’ Wengi wana tabia mbaya zilizozoeleka sana hivyo kwamba hakuna linaloelekea kuwa lenye maana vya kutosha kuweza kuwasukuma wageuze maisha zao. Lakini wengine wa watu hawa wamegeuka wakawa bora. Kwa funzo la Biblia pamoja na mashahidi wa Yehova, wamekuja kufahamu kwamba hali inayofaa mbele za Yehova Mungu inafanya maisha kuwa yenye maana kweli kweli. Hii imewaharakisha wachukue hatua zinazotakiwa ili waipate hali hiyo ifaayo kwa kuzipatanisha maisha zao na sheria ya Mungu yenye haki.

● Mtu mzoevu wa dawa za kulevya katika nchi ya Luxembourg alianza kuona mageuzi ya kweli katika mmojawapo wa rafiki zake na wafanya kazi wenzake. Wakati mmoja rafiki huyu alilewa sana, akavuta sigareti na kujitia katika nyingine zinazoitwa anasa za kilimwengu. Alipoulizwa, rafiki huyo alieleza kwamba alisaidiwa kuzigeuza njia zake kupitia kwa funzo la Biblia pamoja na mashahidi wa Yehova, na mara nyingi aliyazungumza Maandiko pamoja na mfanya kazi mwenzake. Hii ilikuwa na matokeo gani kwa mzoevu huyo wa dawa za kulevya? Yeye mwenyewe anaeleza:

“Vile vile nami nikaamua kuwa na funzo la Biblia. Nyuma ya kujifunza kwa miezi fulani nilitaka kuziacha tabia zangu mbaya na nikaenda kwenye nyumba ya kuugulia wagonjwa kunakoburudishiwa wanaopona. Lakini wakashindwa kuniponya. Nilirudi nyumbani na nikaanza mara moja kujifunza Biblia tena. Nikafahamiana vema zaidi na Mwenyezi Mungu Yehova na karibuni nikaliona pendeleo la kufanya maombi yangu kwake katika sala. Yeye hakushindwa kunisaidia. Nyuma ya mwaka mmoja sikuwa wala mlevi wala mvuta sigareti wala mzoevu wa dawa za kulevya.

“Hapo kwanza mke wangu hakuwa na nia ya kuwasikiliza mashahidi wa Yehova. Lakini nyuma ya kuuona mwenendo wangu uliogeuzwa, yeye vile vile, aliamua kuwa na funzo la nyumbani la Biblia. Tulimwambia mkwe wangu juu ya Maandiko. Yeye aliujua mwenendo wangu wa zamani na kwa hiyo hata yeye alikubali kuwa na funzo la nyumbani la Biblia. Sote watatu tulibatizwa tarehe ya Mei 8, 1971. Mkwe wangu alisema na shemeji yangu juu ya kweli, akikaza fikira zake kwenye mwenendo wangu wa zamani na wa sasa. Leo hata yeye anajifunza Biblia na kuhudhuria mikutano ya mashahidi wa Yehova.”

● Kufanya mageuzi katika maisha ya mtu huenda kukawa na maana ya kuiacha mali. Anasema mwanamke mmoja wa Portugal (Ureno):

“Nilipokuwa mwenye umri wa miaka kumi na minane nilikwenda nikafanye kazi kama mtumishi wa mwanamume mmoja na mkewe waliokuwa matajiri. Sikujua kwamba mke huyo asingeweza kuzaa. Mwanamume huyu na mkewe walitamani sana kuwa na jamaa. Nilitongozwa na kwa miaka mitatu nikamzalia mwanamume huyu watoto watatu. Watoto wangu walilelewa bila ya kukosa cho chote kana kwamba walikuwa wale wa mwanamume huyo na mwanamke niliotumikia. Hivi majuzi, nilijifunza juu ya mashahidi wa Yehova kupitia kwa dada yangu nami nikaanza kujifunza Biblia kwa msaada wa kitabu Kweli Iongozayo kwenye Uzima wa Milele.

“Nyuma ya kujifunza mara ya nne nikajua kwamba ulipaswa uamuzi ufanywe. Nisingeweza kuendelea kuishi katika ufisadi, ikiwa nilitaka kupata baraka ya Mungu na uzima wa milele. Nikaamua kumwacha mwanamume huyu na mkewe nikawalee watoto wangu watatu kulingana na ujuzi wa makusudi ya Mungu. Kwa kuwa nilikuwa mtumishi wa nyumba asiye na mali, wala mume, nililaumiwa na wengi. Wao walisema kwamba watoto wangu wangekuwa na tumaini imara la wakati ujao nikiendelea kuishi na mwanamume yule na mkewe wenye mali. Baba ya watoto wangu akalifikisha shauri hili mahakamani naye akaweza kupata uangalizi wa watoto wawili. Lakini lo! ni mwenye furaha kama nini kuwa niliyapatanisha maisha yangu na mapenzi ya Yehova!”

● Inakuja habari hii kutoka New Zealand: Kule nyuma katika mwaka wa 1969 funzo la Biblia lilianzwa kwa mama wa watoto wanne. Mumewe alipinga vikali. Kisha, kwa sababu ya kuvunja sheria, akafungwa. Kwa kuwa alimshughulikia mumewe, mke huyo alimtumia Mnara wa Mlinzi! na Awake! Mlinzi wa gereza aliyekuwa anajifunza Biblia na mashahidi wa Yehova aliyaona magazeti haya yakifika naye akawajulisha Mashahidi wa kundi la mahali pale. Tangu wakati huo na kuendelea walimtembelea mume huyo kwa kawaida, wakimsaidia kwa upendo asonge mbele katika ujuzi wa kweli wa Neno la Mungu. Hivi majuzi mwanamume huyo alifunguliwa. Mkewe aliutazamia mwungano kwa mara ya pili kwa wasiwasi kidogo. Lakini alipomlaki mumewe katika uwanja wa ndege aliyastaajabia mageuzi yake. Alikuwa amekuwa mtu mwenye fadhili na huruma, akionyesha sifa za Kikristo kweli kweli. Tangu afunguliwe amehudhuria mikutano yote ya Mashahidi.

Kwa kweli matumizi ya kweli ya Biblia yanaweza kuwageuza watu wawe bora.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki